Kibatala amng’ang’ania Luteni Urio kesi ya kina Mbowe

Muktasari:

  • Kiongozi wa jopo la utetezi katika kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu, Wakili Peter Kibatala leo Jumatatu Januari 31,2022 ameendelea kumhoji shahidi wa 12 wa upande wa mashtaka ikiwa ni siku ya tatu mfululizo shahidi huyo kuhojiwa na upande wa utetezi huku mahojiano yakitarajiwa kuendelea kesho.

Dar es Salaam. Kiongozi wa jopo la utetezi katika kesi ya ugaidi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu, Wakili Peter Kibatala leo Jumatatu Januari 31,2022 ameendelea kumhoji shahidi wa 12 wa upande wa mashtaka ikiwa ni siku ya tatu mfululizo shahidi huyo kuhojiwa na upande wa utetezi huku mahojiano yakitarajiwa kuendelea kesho.

Shahidi huyo, Luteni Denis Urio wa upande wa mashtaka ameendelea kuhojiwa na Kibatala katika hatua ya udodosaji

Mchuano baina ya Luteni Urio na mawakili wa utetezi ulianza Alhamisi, baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake wa msingi aliouanza Jumatano ya wiki iliyopita huku akiongozwa na mwendesha mashtaka, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Abdallah Chavula katika Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi.

Leo Jumatatu Kibatala aliendelea kumhoji Luteni Urio kuanzia asubuhi mpaka jioni Jaji Joachim Tiganga alipoahirisha kesi hiyo mpaka kesho Jumanne ambapo Kibatala ataendelea kumhoji shahidi huyo.

Kabla ya Jaji Tiganga kuahirisha kesi hiyo, Kibatala alitoa hoja ya kuomba kesi iahirishe mpaka kesho akidai kuwa bado ana maswali mengi, hoja ambayo iliunga mkono na upande wa mashtaka.


Ifuatayo ni mahojiano baina ya wakili wa utetezi Peter Kibatala na shahidi Luteni Urio


Jaji Joachim Tiganga ameingia mahakamani na kesi inatajwa na karani


Kiongozi wa jopo la Waendesha mashtaka Wakili wa Serikali Mwandamizi, Robert Kidando anafanya utambulisho.


Sasa kiongozi wa jopo la mawakili wa utetezi, Peter Kibatala anafanya utambulisho wa jopo lake.

Jaji Tiganga anawaita washtakiwa kwa kutaja namba zao kwenye kesi kuanzianza kwanza hadi wa nne na wote wanaitika.


Wakili Kidando: Shauri linakuja kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa na Shahidi wetu yupo.


Wakili Kibatala: Nasi Mheshimiwa Jaji tuko tayari


Sasa Wakili Kibatala anaanza kumhoji shahidi. Shahidi huyo, Luteni Denis Urio wa upande wa mashtaka.


Wakili: Mhe Urio good morning


Shahidi: Morning too


Wakili:  Naendelea kukuuliza maswali. Ukiacha tukio hili umewaji kukutana na tikio longine kubwa la kigaidi kama hili?


Shahidi: Hebu rudia


Wakili: Ulishawahi kukutana na mtu mnayefahamiana akakwambia matukio mazoti kama haya au ni mara yako ya kwanza?


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Ulisama huna matatizo ya kumbukumbu?


Shahidi: Sahihi


Wakili: Sasa Shahidi inawezekana vipi ukasahau tarehe muhimu kama hizi za tarehe ya kukutana na Mbowe kukwambia masuala haya na tarehe ya kwenda kwa DCI na hasa Askari mkubwa kama wewe mwenye cheo cha Luteni?


Shahidi: Ni mara ya kwanza kupata taatifa kama hizo kwa Mheshimiwa Mbowe hivyo sikuamini mara moja lakini angekuwa na rekodi kama hizo ningejua.


Wakili: Vipi kukumbuka kwenda kwa DCI?


Shahidi: Sijakumbuka kwa sababu si duty yangu ya kufanya uchunguzi.


Wakili: Sawa, unaweza kusaidia kwa nini hata DCI katika maelezo yake hakumbuki?


Shahidi: Siwezo kumjibia DCI


Wakili: Unafahamau au hufahamu?


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Je kwa nini hata ACP Kingao ambaye alikuwepo naye hafahamu?


Shahidi: Sijui kwa nini hajui


Wakili: Na kuhusu ofisa mwingine wa Polisi, Afande Swila naye hafahamu?


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Wewe unaona hii hali ni ya kawaida?


Shahidi: Nilikwenda ofisi ya mtu sasa siwezi kumlazimisha kutake note.


Wakili: Unafahamu kwa nini maelezo yako yaliandikwa karibu mwezi mmoja baadaye badala ya kuwa ya kwanza?


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Huoni kwamba ni busara maeelezo ya mtu muhimu kama wewe mtoa taarifa kuandikwa mapema?


Shahidi: Sielewi utaratibu wake yeye kama anaona inafaa


Wakili: DCI alikufafanulia kwa nini maelezo yako hayakuchukuliwa mapema?


Shahidi: Hawakunifafanulia


Wakili: Tarehe 11/8/2020 ndio ulikwenda kwa Inspekta Swila kuandika maelezo yako ya tukio zito la kupanga njama na makomandoo, Swila alikufafanulia?


Shahidi: Hakunifafanulia


Wakili: Tukiamini kwamba tuhuma zilitungwa kwanza ndipo wakatafutwa washtakiwa tunakuwa tunakosea?


Shahidi: Utakuwa unakosea.


Wakili: Katika kikao chenu wewe DCI na Kingao mliwahi jadili mbinu ya kumtuma Askari wa Polisi aende kwa Mbowe ajifanye ili kupata ushahidi kwa sababu wao wako trainees na wana vifaa?


Shahidi: Mimi sikuwahi kujadili


Wakili: Ni kweli kwamba katika ushahidi wako kuwa Mbowe alisema anataka kuchukua dola kwa namna yoyote na gharama yoyote kwenye uchaguz wa 2020


Shahidi: Ni kweli


Wakili: Na Bado unasisisitiza kwamba kwa hizo factor wewe hukuwa ni mwanajeshi kazini na wanaotakiwa Ni X Commandos bado jeshi halikujitaji kuchukua hatua?


Shahidi: Kwa sabau ni taarifa zilizotolewa kwenye uraia kwa hiyo bado zingerudi polisi maana ni taarifa ambazo hazikuwa sahihi.


Wakili: Unamfahamu aliyekuwa Luten Shimbo?


Shahidi: Namfahamu


Wakili: Kwamba Oktoba 13, 2010 Luten Shombo alisema kuwa uchaguzi unakuwa wa amani na kwamba Jeshi  liko tayari kuchukua nchi kama kungetokea uvunjifu wa amani


Shahidi: Sikuwahi kusikia


Wakili: Kwa nini Hamkuona kwa taarifa hizo ambazo zinawahusisha makomandoo mngetuma makomandoo kuwa kama mamluki?


Shahidi: Kwanza Mbowe alikuwa hapokei simu na aliomba picha zao ili afanya research kama wako kazini.


Wakili: Kwa hiyo Freeman Mbowe ana mbinu za kufanya cross checking za Askari?


Shahidi: Ndio, kwa nini alitaka picha zao, kwa nini alitaka kujua umri wao


Wakili: Katika ushahidi wako ulisema Mbowe ana access na mtu mwingine jeshini?


Shahidi: Sikusema


Wakili: Kwa hiyo ni kweli kwamba kuna mambo ulikuwa huyafahamu hujui kama Mbowe alikuwa na plan A na B?


Shahidi: Ndio


Wakili: Unasema hukuwa na uhakika kama Mbowe alikuwa na plan A na B na Mbowe alikuwa na trust na wewe ulimhoji kama alikuwa na mtu mwingine ambaye alikuwa ameshamu-approach?


Shahidi: Sikumhoji


Wakili: Kwa assessment yako alikuwa anakuamini?


Shahidi: kuwa alikuwa ananiamini Mimi peke yangu?


Wakili: Na unasema alikuahidi cheo Kikubwa jeshini kama?


Shahidi: Kwa mawazo yake yeto, Mbowe hawezi kunipa cheo


Wakili: Baada ya kuachana na Mbowe mawazoni mwako ulikuwa umeshamkubalia au kumkatalia?


Shahidi: Kumkatalia


Wakili: Na kweli wakati anakwambia ulikuwa unamsikiliza tu na kwawmba ngoja amalize tu nakwenda kutoa taarifa?


Shahidi: Kuna hatua…


Wakili: Akili ya kawaida ya Luteni haikuweza kum-probe ili iujua huyu anapanga kulipua vituo vya mafuta au ni viongozi gani?


Shahidi: Kwa akili ya kawaida hata kama ni wewe ukishaanza kumdodosa anastuka.


Wakili: Utakubaliana na Mimi kwamba neno lako wewe dhidi ya neno la Mbowe na hakuna ushahidi wa sauti wala hamkutuma decoy?


Shahidi: Ndio maana tulituma hao vijana


Wakill: Hawa Ni washtakiwa kwani hawa ni mashshidi wenu?


Shahidi: Waliiingia kwenye uhalifu wenyewe


Shahidi: Unakumbuka lini uliongea na Ling'wenya?


Shahidi: Sikumbuki


Wakili: Ni kweli kwamba mzee Ling'wenya alikuwa aataka umwachia mwanaye kuhusu hiyo kazi kutokana na historia ya yale yaliyotokea jeshini?


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Una ugomvi na mzee Ling'wenya mpaka akutungie hayo?


Shahidi: Sitahamu na wala sijawahi kumuona


Wakili: Unatajambua kuwa mzee Ling'wenya moyo wake unavuja damu kwa haya anayopitia kwa  mwanaye uliyemuomba kuwa unamtafutia  kazi ?


Shahidi: Sifahamu, kwani mwanaye aliambiwa kwamba akashiriki uhalifu?


Wakili: Alipokuuliza kuhusu mwanaye kukamatwa ulimpa ushirikiano gani?


Shahidi: Nilimwambia aongee na bosi wake.


Wakili: Ulimweleza mzee Ling'wenya ukweli kwamba Mbowe ana mipango ya ugaidi kwa hiyo tunataka kumtumia mwanao ili kupata ushahidi?


Shahidi: Sikumwambia


Wakili: Umeshawahi kusikia neno kumtoa mtu kafara?


Shahidi: Nafahamu


Wakili: Siku ya kwanza nilikuuliza maswali mengi kuhusu kwenda kanisani ukasema wewe ni Mkristo, Unamfahamu Daniel kwenye Biblia?


Shahidi: Namfahamu


Wakili: Unafahamu walichomfanyia?


Shahidi: Nafahamu walimtupa kwenywe tundu la Simba


Wakili: Unafahamu kwanza walimuingiza kwenye mtego kwa kumwambia atunge sheria, Mkristo mwenzangu huoni kuwa hicho ulichomfanyia mzee Ling'wenya kinafafana na hicho alichofanyowa Daniel?


Shahidi: Ni tofauti kabisa


Wakili: Na Mkristo mwenzangu moyo wako uko sawa tu?


Shahidi: Sawa kabisa


Wakili: Unafajamu mzee Ling'wenya ametumikia nchi hi bila doa?


Shahidi: Sifahamu



Wakili: Ni mazingira gani kiongozi anaweza kuondoka na kuwaacha askari wake


Shahidi. Huwezi kukaa sehemu moja na wafuasi wako wafuasi wanatakiwa kukaa mbele na kiongozi nyuma


Wakili. Unafahamu Adam Kasekwa aliachishwa kazi kwa kupata tatizo la kisaikolojia


Shahidi. Hana historia hiyo


Wakili. Kwenye maelezo mliyoleta mnasema ana historia hiyo


Shahidi. Kwani ameleta cheti cha daktari


Wakili. Ulifahamu sababu mahususi ya Ling'wenya kuachishwa kazi


Shahidi. Kwa utovu wa nidhamu


Wakili. Kwa kuwa uliwasiliana na Bwire unafahamu ni maeneo gani mahususi walitembelea kwaajili ya kumdhuru Sabaya


Shahidi. Bwire hakuniambia


Wakili: Unafahamu allegation ilikuwa ni kumdhuru Sabaya kwenye maeneo hayo


Shahidi: Aliieleza in breif lakini hakuniambia ni maeneo gani


Wakili. Nani aliyetumwa kumtafuta Mbowe ni nani


Shahidi. Ni mimi


Wakili. Mbowe aliomba polisi wamtafutie vijana


Shahidi: Hakuomba


Wakili: Ni kweli uliandika maneno hayo katika maelezo yako


Shahidi: Ni kweli


Wakili: Polis walikuwa na mawasiliano na Bwire


Shahidi; Hawakuwa nayo


Wakili:  Nani alikuwa anaaminiwa na Bwire na Adamoo


Shahidi: Ni mimi


Wakili: Kuna msiri alikuwa anawapa wakina Kingai taarifa na kueleza walivyovaa ni wewe


Shahidi: Sio mimi


Wakili: Kingai aliwahi kukwambia kuna msiri wao mwingine zaidi yako


Shahidi: Hapana


Wakili: Kuna mtu mwingine alikuwa anawafahamu kadri waeleze walivyokuwa wamevaa


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Unafahamu walichokuwa wanafanya pale Rau Madukani


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Unafahamu Ling'wenya ana dada yake pale Rau madaukani walikuwa wameenda kumsalimia


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Unafahamu Ling'wenya ana dada yake anaishi Sakina Arusha


Shahidi: Haikuwahi kuniambia


Wakili: Kati maelezo yako uliandika ulimpa Kingai namba za simu ili aweze kuwa fuatilia


Shahidi. Ni sahihi


Wakili. Wakati unaaongozwa na wakili uliongelea kuwa ulimpa Kingai namba za simu


Shahidi. Sikuongelea


Wakili. Ni muhimu au sio muhimu


Shahidi. Ni muhimu

Wakili. Unafahamu maana yake kuzungumzia suala la namba ya simu


Shahidi. Sifahamu


Wakili. Unafahamu nama ndugu walivyohangaika kuwatafuta ndugu zao kwenye vituo vya polisi na hospitali


Shahidi. Sifahamu


Wakili: 11/8/2020 uliandikishwa maelezo na kumkabidhi simu zako wakati Swilla anachukua simu yako alikuruhusu kutoa line


Shahidi. Ni sahihi


Wakili. Ulimwambia Jaji kuwa uliondoka na simu line yenye mawasiliano yako


Shahidi: Kulikuwa na line mbili


Wakili: Line ya Vodacom ulimwambia Jaji tarehe 12 uliirusha


Shahidi: Nilimwambia


Wakili: Hiyo nakala ya makabidhiano ya line ya voda ulikuja nayo


Shahidi: Sikujua kama itahitajika mahakamani


Wakili:  Tukiomba tukague simu kama line ipo?


Shahidi. Vyovyote itakavyowezekana


Wakili. Mheshimiwa Jaji naomba kielelezo namba 34


Wakili Kibatala anampa Shahidi simu aiwashe ili wakague laini iliyopo.


Shahidi: Hakuna line hata moja


Wakili: Unajua maana ya kiapo chako


Shahidi: Nafahamu


Wakili: Unajua ukweli na uongo unapimwa kwa vitu vidogo vidogo kama hivi


Shahidi: Nafahamu


Wakili:Wakati unaamkabidhi Inspekta Swilla simu ilikuwa na line


Shahidi: Ndio ya Airtel


Wakili: Iko wapi


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Ushahidi wako wa mdomo ulimkabidhi Swilla simu tatu utaungwa mkono na nini


Shahidi: Kwa sababu ziko hapa


Wakili: Unafahamu simu hizi tatu ni za muhimu kwa kuwa zilikuwa na mawasiliano flani


Shahidi: Nafahamu


Wakili: Ulimwambia Jaji simu mbili ulizozifuata uliziacha kwa nani


Shahidi: Nilimwambia


Wakili: Ulimwambia uliziacha chini ya uangalizi wa nani


Shahidi: Sikumwambia


Wakili: Unafahamu ni kwanini kataika maelezo ya Inspekta Swilla hazungumzii simu tatu

Shahidi: Sihitaji kufahamu


Wakili: Unafahamu Freeman Mbowe alikuwa na kaka mwenye cheo kikubwa jeshini na Rais Magufuli alihudhuria Msiba huo


Shahidi: Nilisikia


Wakili: Unataka tuamini Mbowe alimuacha kaka yake wa damu akakutafuta wewe


Shahidi: Alishastaafu


Wakili: Wewe na General nani anafahamu watu wengi zaidi


Shahidi: Yeye


Wakili: Unasema ulishangaa mara ya kwanza Mbowe kukupiga simu


Shahidi: Ndio


Shahidi: Unafahamu mtu kuwa na mawasiliano yako unaweza kulalamika


Shahidi: Mimi sio mtu wa muhimu


Wakili: Unafahamu mtu kukusumbua unaweza kulalamika


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Ulitoa taarifa


Shahidi: Sikutoa taarifa


Wakili: Katika maelezo yako uliandika ulikuwa na ukaribu na Mbowe kwa kuwa ni kabila moja


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Nini kilikupa comfort hadi ukaendelea kuwasiliana naye


Shahidi: Mbowe ni Mbowe na Chama ni Chama


Wakili: Katika maelezo yako ulitenganisha


Shahidi: Sikutenganisha


Wakili: Unasema ulitumiwa 500,000 ukatoa 300 000 ukabakiwa na 200,000


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Unakumbuka ulichoandika katika maelezo yako


Shahidi: Nakumbuka


Wakili: Katika maelezo yako umesema ulipopokea ulizitoa zote


Shahidi. Hapana sikuzitoa


Wakili. Unakubaliana na mimi ulitoa 300000 na 200000 zikabaki kwenye simu


Shahidi. Ni sahihi


Wakili. Uliambiwa maana ya haya maelezo


Shahidi: Sikuambiwa


Wakili: Hakuna mahali uliposema hii hela zote ulizitoa mfukoni


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Utakubaliana na mimi ulichokisema na kilichaoandikwa vinatofautiana


Shahidi. Ni sahihi


Wakili: Ulimwambia Jaji 40000 ilienda wapi?


Shahidi: Sikumwambia


Wakili: Katika maelezo yao wanasema uliwapa Sh 87, 000 kila mtu?


Shahidi: Sikumpa mmoja mmoja hela


Shahidi: Kwahiyo katika haya maelezo na unacho sema wewe ni tofauti


Shahidi: Ni tofauti


Wakili: Unakubali au unakataaa jumla ni Sh174, 000


Shahidi: Amount hiyo siwezi kuifahamu


Wakili: Ushahidi huu na wako unatofautiana?


Shahidi: Unatofautiana


Wakili: Fedha ulizotumiwa na Mbowe ilikuwa kuwagharamia nauli zao za kuja Morogoro


Shahidi: Ni sahihi

Wakili: Naomba nikusumbue tena Shahidi nisaidie kuwasha kielelezo namba 34 uende kwenye meseji ambazo ulizisoma

Shahidi: Tayari

Wakili: Ni kweli ulisema Mbowe alikuambia umtafutie makomandoo wasiokuwa na kikomo

Shahidi: Hakuniambia idadi


Wakili: 20/7/2020 meseji inasema idadi ni watatu au wanne


Wakili: Hebu isome kwanza


Shahidi: Kaka wale mtu tatu au nne ni muhimu siku zimeisha


Wakili: Hapa anataja mtu tatu au nne


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: 20/7/2020 saa 2:3 hii meseji nani alituma


Shahidi: Mimi nilituma kwenda kwa Freeman Mbowe


Wakili: Hii ilituma kwa namba gani


Shahidi: Mtandao wa Telegram


Wakili: Ili iweze kusajili mtandao wa telegram si lazima uwe na simcard


Wakili: Ulitumiwa namba gani msomee Jaji asikie


Shahdi: 1130138344


Wakili: Imeandikwa owner Denis Urio


Wakili wa Serikali Mwandamizi Pius Hilla. Sio nia yetu kusimama Wakili kamwambia asome Shahidi kasoma lakini wakati anataka kutoa ufafanuzi Wakili hataki.

Wakili Kibatala: Mheshimiwa Jaji hiyo namba wameileta wao hawakutoa ufafanuzi anataka kufanya submission watatakiwa wamuulize Shahidi kwenye re examination

Jaji: Kama nimemsikia vizuri Kibatala anamuuliza Sahahid kama anaifahamu hiyo namba kabla ya kujibu akawa anataka kutolea ufafanuzi lakini kwenye cross examination shahidi anatakiwa kujibu kile anachoulizwa.

Wakili Kibatala: Hiyo namba unafahamu


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Kuna mtu alikuongoza kufafanua hiyo namba


Shahidi: Hakuna


Wakili: Unafahamu application inaitwa Freeman sms


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Kuna mtu alikuongoza au kukuuliza kama unafahamu free sms


Shahidi: Hakuna


Wakili: Simu yetu bado ina chaji


Shahidi: Ndio


Wakili: Kuna sehemu yoyote Mbowe anakwambia kutumia simu sio salama


Shahidi: Yah mwisho


Wakili: Isome


Shahidi: Hello bro nimeshindwa kupokea simu kwa sababu ya......


Wakili: Kwahiyo unataka kusema imefanana na hiyo usitumie simu sio salama sana


Wakili: Linganisha meseji uliyomsomea Jaji na hii hapa zimefanana?


Shahidi: Zinafanana


Wakili: some Jaji


Shahidi: 729414989


Wakili: Inasemekana ni ya nani


Shahidi: Free


Wakili: Zinafanana na za kielelezo ulichosaoma awali


Shahidi: Zinatofauti kubwa

Wakili: Tafuta sms ya tarehe 20/7/ 2020 ya saa 2:14 isome


Shahidi: Naomba nitumie nauli niwamobilize nikutane nao Morogoro


Wakili: Nani alikuwa anaomba nauli


Shahidi: Mimi


Wakili: Baada ya wewe kuomba nauli Mbowe ndio akatuma


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Nitafutie meseji ambayo Mbowe anatoa wazo la kutuma hiyo 500,000


Shahidi: Hakuna

Wakili. Ni nani kwa mujibu wa meseji aliyetoa wazo la kutuma 500,000


Shahidi: Ni mimi


Wakili: Kwa mujibu wa kielelezo namba 34 hiyo meseji ulituma kwa kutumia namba gani


Shahidi: Haionekani


Shahidi: Tafauta meseji ya tarehe 20 /7/2020


Shahidi: Nimeiona


Wakili: Usiwe unatumia namba yako kutuma pesa tumia Wakala au wasaidizi wako, Ni nani alituma ujumbe huu?


Shahidi: Ni mimi kwenda kwa Freeman Mbowe


Wakili: Hao wasaidizi waliwahi kukutumia pesa kutumia namba zao


Wakili: Unamfahamu msaidizi wa Mbowe anaitwa Wile


Shahidi: Sifahamu


Wakili:  Kwenye mazungumzo yenu kwenye miamala ya kifedha hajawahi kuzungumzia mtu anaitwa Wile

Shahidi: Nimewahi

Mahakama imerejea baada ya mapumziko ya muda mfupi kwaajili ya Wakili wa utetezi Peter Kibatala kuendelea kumuhoji shahidi wa 12, Luten Denis Urio.


Mawakili wa pande zote wako tayari kuendelea


Wakili Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba kielelezo namba 34 na 36


Wakili: Shahidi washa simu

Shahidi: Tayari

Wakili: Meseji ya tarehe 22/7/2020 saa 3:19:30 Namba ya dereva wangu anaitwa Wille atatuma pesa na ndio atawapokea ni sahihi

Shahidi: Ni sahihi

Wakili: Tarehe hiyo namba iliyotuma pesa iliingia kwenye simu yako


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Ni wapi unasema Freeman Mbowe alikutumia hiyo namba


Shahidi: Alituma kwa njia ya kawaida


Wakili: Iko wapi


Shahidi: Sikumbuki


Wakili: Huyu Wille hujawahi kukutana naye


Shahidi: Sijawahii kukutana naye


Wakili: Huyu Mbowe alikwambia umtafutie watu au magaidi


Shahidi: Kwaaji ya kwenda kuambatana naye na kufanya nchi isitawalike


Wakili: Kwahiyo wewe ulikuwa unamtafutia Mbowe watu kwaajili ya kufanya uhalifu


Shahidi: Walinzi


Wakili. Waliwahi kukwambia wakina Kingai unatakiwa uwe mshtakiwa namba moja au mbili

Shahidi. Hawakuwahi kuniaamba


Wakili: 22/7/2020 saa 12:27 hiyo sms nani alituma


Sahahid: Mimi kwenda kwa Freeman Mbowe


Wakili: Wakina Bwire walikuwa wameshaindoka kwenda kwa Mbowe


Shahidi: Ni sahihi

Wakili: Kwa maelezo haya inamaana ulitoa zote kwa pamoja


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Ushahidi wako na maelezo ni sahihi vinatofautiana au vinapishana


Shahidi: Vinaoana tofauti iko kwenye tafsiri

Wakili:  Ulikuwa unashauri Mbowe awe anakutumia fedha za ziada


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Kwahiyo ulikuwa unamuomba ukijua anamipango ya kigaidi


Shahidi: Ni sahihi

Wakili: Ulishawahi kusikia neno soulitationi


Shahidi: Sijawahi


Wakili. Fedha hizi ulikuwa unaomba baada ya kupokea 500,000


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Ulisema kila hatua ulikuwa unamfahamisha Kingai


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Unaweza kutuonyesha meseji yoyote uliyomtumia Kingai


Shahidi: Hakuna


Wakili: Na meseji yoyote unayotumiwa fedha


Shahidi:  Hakuna

Wakili: Kuna meseji inasomeka Shkamoo Mkuu


Shahidi: Ni sahihi


Wakili. Kwahiyo ulikuwa unamsalimia mtu anayeenda kutekeleza vitendo vya kigaidi


Shahidi. Ndio nilikuwa sina ugomvi naye


Wakili: Unasema Halfani Bwire alikupigia akakwambia wenzake wako Moshi wanaenda kutekeleza vitendo vya Kigaidi


Shahidi: Hakunipigia mimi ndio nilimpigia


Wakili: Katika maelezo yako uliandika kuwa wako Moshi wanampango wakumshambulia Sabaya


Shahidi: Mimi nilimpigia


Wakili. Unataka tuamini ulichokiandika Bwire naye yuko Moshi


Shahidi: Tumuulize


Wakili: Na katika maelezo yako uliandika Bwire yuko Dar es Salaam


Shahidi: Sikuandika


Wakili: Katika maelezo yako umeandika tukakutana tena na Freeman Mbowe limeingizwa kimakosa kwa sababu umesaini na kudthibitisha kuyasoma?


Shahidi: Sahihi


Wakili. Unasema kabla ya kukutana naye alikuwa anakutumia na ujumbe na kukutakia heri?


Sahahidi: Ni sahihi


Wakili: Mtu anayekutumia ujumbe na kukutakia heri ni mzalendo au sio mzalendo


Shahidi: Ni mzalendo

Wakili: Nani alikutafuta ni Freeman Mbowe au wewe ulimtafuta


Shahidi: Yeye ndio alinitafuta


Wakili: Kupitia nini


Shahidi: Simu na kupitia Whatsup call na namba nyingine


Wakili: Hizo namba ulizifikisha kwa DCI


Shahidi: Sikuzifikisha


Wakili: Nani aliandika maelezo yake kuwa nilimtafuta na kumwambia kuwa tunaweza kuonana.

Kuna sehemu umeandika kuwa ulimtafuta baada ya kukuita micdcall


Shahidi: Hamna


Wakili: Unaona kuna mfanano hapo au kuna tofauti


Shahidi: Kuna tofauti


Wakili: Kuna mahali ulipoandika kuwa baada ya kumpiga. DCI ulijutambulisha kama Ofisa wa jeshi


Shahidi: Nilijitambulisha


Wakili: Mheshimiwa Jaji kwa Ruhusa yako naomba wenzangu wanipe nyaraka halisi ya maelezo


Wakili: Maelezo ni ya kwako


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Nitafutie hiyo sehemu tafadhali


Shahidi: Hakuna


Wakili: Maelezo yako na ushahidi wako vinafana


Shahidi: Vinatofautiana


Wakili: Unakumbuka ulichojibu kwa wakili Mallya kuhusu kutumiana meseji


Wakili Kidando: Mheshimiwa Jaji naomba Shahidi asome maelezo yake kwanza


Wakili Kibatala: Mheshimiwa Jaji nyaraka hii inasomwa baada ya kuingia


Jaji: Utaratibu unasema nyaraka kwanza isomwe


Wakili Kibatala: Haya Shahidi soma maelezo yako.


Wakili: Ngerengere na Kihonda pana umbali gani


Shahidi: Kilomita 50 au 60


Wakil: Ulishamwambi Mheshimiwa Jaji unaishi Kihonda


Shahidi: Familia yangu iko kule


Wakil: Ulishawahi kusema hapa mahakamani kama kuwa unaishi Kihonda


Shahidi: Hapana


Wakili: Una matatizo na hayo maelezo


Shahidi: Hapana


Wakili: Unataka Jaji atende haki kabisa


Shahidi: Ndio


Wakili. Kuna tatizo tukiyatoa


Shahidi: Hakuna tatizo


Wakili. Mheshimiwa Jaji kama Shahidi alivyoomba


Jaji: Upande wa mashtaka mnasemaje


Wakili Kidando: Hatuna pingamizi Mheshimiwa


Jaji. Mahakama imepokea maelezo haya kama kielelezo namba nne cha upande wa utetezi.

Wakili: Shahidi simu bado ina chaji?


Shahidi: Ngoja niwashe


Wakili: Kuna meseji inasema kuwafanyia vetting ilikuwa vetting ya nini?


Shahidi: Kwa kuwa wanaenda kufanya kazi ya ugaidi ni muhimu kufanya vetting na wakiona vitendo vya kihalifu waniambie


Wakili: Hii meseji ulikuwa unajitumia mwenyewe au?


Shahidi: Nilikuwa natumia Freeman Mbowe


Wakili: Kuna kitu kingine cha ziada ulitaka kuwafanyia wakina Adamoo hadi ukaomba hela ya ziada kwa Mbowe.


Shahidi: Kwa kuwa hela ya awali ilishakuwa comshumd


Wakili: Ulikuwa unawafanyia orientation magaidi.


Shahidi: Ndio kwa fedha za Mbowe


Wakili: 22/7/2020 ulituma meseji inasema lakini wewe usitumie namba yako nani alituma


Shahidi: Mimi kwenda kwa Freeman Mbowe


Wakili: Kwa nini ulimtumia


Shahidi: Ili kuongeza Trust


Wakili: Nauli pamoja na hela za kula ni 2000, 000 nani alituma hiyo meseji


Shahidi: Mimi kwenda kwa Mbowe


Wakili: Hapa mlikuwa mnakubaliana nini kuhusu mishahara


Shahidi: Kwa hiyo kazi wanayoenda kuifanya


Wakili: Ni kazi gani hiyo


Shahidi: Ya uhalifu


Wakili: Kuna meseji inasema kuhusu utawala utawala ni nini


Shahidi: Chakula


Jaji: Nimepata taarifa kuna mafundi wanahitaji kufananya matengenezo tujitahidi angalau saa kumi na nusu tumalize.

Wakili Kibatala: Basi ngoja nisukumesukume hadi hapo kisha ntatoa hoja ya kuahirisha.


Wakili Piusi Hilla. Mheshimiwa Jaji tunaomba Wakili afanye cross kuna maeneo naona anarudia


Jaji. Ni vizuri unapouliza maswali ukatoa eneo hilo moja badala ya kurudia rudia.


Wakili Kibatala: Kama kuna sehemu anaona nimerudi au kama kuna swali basi aseme.

Wakili: Unaweza kufanya mlipuko bila kuwa na vya kulipiulia


Shahidi: Huwezi


Wakili: Katika ushahidi wako kuna sehemu ulisema bunduki aina ya luger ni mahusi kwaajili ya makomandoo kufanya ugaidi


Shahidi: Sijasema


Wakili. Baada ya Julai 24, 2020 uliwahi kuwasiliana tena na Mbowe


Shahidi: Nilikuwa nikimpigia hapokei nikamtumia meseji


Wakili: Ulikuwa unawasilia naye kwa meseji


Shahidi: Telegram


Wakili: Ulimuonyesha Jaji meseji ulizokuwa ukifanya juhudi za kumtafuta Mbowe


Sahahid: Sikufanya


Wakili: Tunakubaliana kilichoandikwa hapo ni simu yako na sio simu zako


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Uliongozwa na wakili wa Serikali kuonyesha rekodi zako za simu ulizokuwa unawasiliana na Bwire


Shahidi: Hapana


Wakili: Inspekta Swilla alikwambia na yeye ni mpelelezi kwenye shauri hili


Wakili: Sifahamu


Shahidi: Ni sahihi hukuwahi kusema kama uliandika maelezo ya ziada


Shahidi: Ndio


Wakili: Kambi ya makomandoo ipo Ngerengere au Kizuka


Shahidi: Kizuka


Wakili: Ulimwambia Jaji kuwa Kambi iko Kizuka na sio Ngerengere


Shahaidi: Ngerengere ni tarafa


Wakili Kibatala: Unakuambuka nilikwambia nini kuhusu namba DCI


Shahidi:  Nakumbuka


Wakili: Ulisemaje


Shahidi: Nimeacha hotelini kwangu kwenye diary


Wakili: Ijumaa tulivyoachana hapa hadi leo na hujaja nayao


Shahidi:  Nilisubiri nipewe maelekezo na mahakama


Wakili: Na wakili Mallya alikuuliza kuhusu Order nayo iko wapi


Shahidi: Hotelini kwangu


Wakili: Kwahiyo na leo nikihitaji haipo.

Wakili: Kipindi kinachohusiana na shauri hili ni kuanzia Juni 2020 hadi Agosti 2020


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Mbowe alikuwa anawasiliana na wewe kwa Telegram ili kuficha mawasiliano yenu


Shahidi: Ni sahihi


Wakili: Kabla ya tarehe hizo tukiangalia hatutakuta mahali mlikuwa mnawasiliana kwa telegram kabla ya tarehe hizo

Shahidi: Tulikuwa tunawasiliana kwa whatsup


Wakili. Ulimwambia Mheshimiwa Jaji wakati unamkabidhi Inspekta Swilla simu ulimuona akibandika kikaratasi


Shahidi: Sikumwambia


Wakili: Kazi ya kuzuia uhalifu ni yako au polisi


Shahidi: Polisi


Wakili: Chakula alichokula Adamoo na wenzake nani alilipia


Shahidi: Kililipiwa na pesa za Freeman Mbowe


Wakili: Ulisema katika fedha ulizowapa wakina Adamoo walitoa kiasi flani kwaajili ya chakula


Shahid: Sikusema


Wakili: Unafahamu hakuna simu ya Mbowe hata moja iliyokamatwa


Shahidi: Sifahamu


Wakili: Wewe ulikuwa una mamlaka yoyote ya kiupelelezi zaidi ya kutoa taarifa?


Shahidi: Sina mamla ya kiupelelezi zaidi ya kuto taarifa


Wakili Kibatala: Mheshimiwa Jaji bado nina maswali kwa shahidi na kupitia ombi letu naomba tuahirishe kesi hadi kesho Februari Mosi, 2020 kwaajili ya kuendelea na Cross Examination.


Wakili Kidando: Hatuna pingamizi Mheshimiwa iIa tunaomba Shahidi kesho ajielekeze kwenye maeneo ambayo hayajaulizwa.


Jaji: Naahirisha kesi hii hadi kesho Februari Mosi 2022 kwaajili ya shahidi wa 12 kuendelea kuhojiwa na upande wa utetezi.

Shahidi unakumbushwa kuja kuendelea kutoa ushahidi wako washtakiwa mtaendelea kuwa chini ya uangalizi wa Magereza.