Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kichwa chazikwa baada ya mwili kuliwa na mamba mtoni

Muktasari:

  • Mwanamke azikwa kichwa baada ya mwili wake kuliwa na mamba katika mto Lukuredi katika kijiji cha Nachui wakati alipoenda kuoga na kuchota maji katika ambapo masalia ya mwili wake yalipatikana baada ya siku tatu.

Lindi. Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi limetoa taarifa ya mwanamke mmoja mkazi wa kijiji cha Nachui Kata ya Nyengedi Halmashauri ya Mtama mkoani Lindi akidaiwa kufariki dunia baada ya kuliwa na mamba katika mto lukuredi.

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi, ACP Alhaji Salim Kabaleke ambaye amethibitisha kutokea kwa tukio hilo Mei 24, 2023 katika mto Lukuledi uliopo Kijiji cha Nachui.

Alisema kuwa mwanamke huyo aliyefahamika kwa jina la Somoe Saidi (65) alienda kuoga katika mto huo na kuchota maji ndipo alipokumbwa na madhira hayo.

Kwa mujibu wa kamanda huyo inasemekana kuwa siku ya tukio mama huyo alikwenda mtoni kwa ajili ya kukoga na kuchota maji lakini baada ya muda kupita wanakijiji wengine walikwenda mtoni ndipo wakakuta ndoo ya maji pamoja na nguo pembezoni mwa mto huo bila kuwapo na mtu hali ambayo iliwapa mashaka kwakuwa waliona michirizi ya damu pembezoni mwa mto.

ACP Kabeleke alisema kuwa mwili wa marehemu ulipatikana siku ya tatu baadaye baada ya kufanya msako kwa kushirikiana na askari wa maliasili huku mwili wake ukiwa umeliwa na mamba na kusalia kichwa pekee.

"Jeshi la Polisi limewataka wakazi wanaoishi na kufanya shughuli zao karibu na mto Lukuledi kuwa makini na mamba huku akiwaomba kushirikiana na watu wa maliasili ili kutambua maeneo hatarishi ya makazi ya mamba hao,” amesema ACP Kabeleke.