Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mafuriko yawakosesha makazi watu 90 mkoani Manyara

Muktasari:

Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimesababisha Ziwa Bassotu wilayani Hanang' Mkoa wa Manyara kujaa na maji kwenda katika makazi ya watu.

Hanang'. Mvua zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimesababisha Ziwa Bassotu wilayani Hanang' Mkoa wa Manyara kujaa na maji kwenda katika makazi ya watu.

Amesema hali hiyo imesababisha wakazi 90 wa Wilaya hiyo kukosa makazi.

Mbali na kukosa makazi, mawasiliano ya Wilaya ya Hanang' na Mbulu yamekatika baada ya barabara ya Katesh-Haydom kutopitika.

Mmoja wa wakazi wa kijiji hicho, Jackson John amesema  kwa sasa wanaishi kwa ndugu na jamaa na majirani.

"Hizi mvua zinazoendelea kunyesha ni kubwa zaidi ya zilizonyesha hivi karibuni kwa sababu zimesababisha  madhara makubwa kwetu tunaoishi karibu na ziwa," amesema.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Manyara, Paul Kasabago amesema aliagiza barabara ya Katesh-Haydom isitumike kwa lengo la kuepusha madhara.

Amesema hivi sasa barabara hiyo ni hatari kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha kusababisha madaraka kukatika.

"Nimewaagiza askari wa kituo cha polisi Bassotu kuzuia matumizi ya barabara hiyo hadi wataalamu watakaporuhusu ili kuepusha ajali zisizo na lazima," amesema Kasabago.

Diwani wa Bassotu,  Samuel Qawoga amesema hivi sasa wananchi hao 90 wanasaidia vyakula na majirani.