Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mwanamke ‘aliyekufa’ akutwa hai mochwari

Muktasari:

Mwanamke huyo alipatikana akiwa hai kwenye chumba cha kuhifadhia maiti


Mwanamke mmoja nchini Afrika Kusini amezua taharuki baada ya kupatikana akiwa hai katika jokofu la kwenye chumba cha kuhifadhia maiti.

Mwanamke huyo alifikishwa katika chumba hicho baada ya madaktari kusema alikuwa amefariki dunia kufuatia ajali ya barabarani.

Katika uchunguzi wao madaktari walisema hakuonyesha dalili zozote za kuwa hai na hivyo kutamka kuwa alikuwa amepoteza maisha.

Mafundi wanaofanya kazi katika chumba hicho ndio waliogundua kuwa mwanamke huyo alikuwa hai na hatimaye kumwondoa.

Aliletwa kwenye chumba hicho akidhaniwa amepoteza maisha yeye na wenzake wawili baada ya gari walilokuwa wakisafiria kupinduka na kuvingirika zaidi ya mara tatu.  Wawili hao waliobakia ndiyo waliofariki dunia.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la AFP, mwanamke huyo ambaye hakutajwa jina lake sasa amekuwa akipokea matibabu katika Hospitali ya Leratong iliyoko Magharibi mwa mji wa Johannesburg.

Familia ya mwanamke huyo aliyegunduliwa kuwa hai imesema wamepata mshtuko na wana wasiwasi mkubwa kuhusu mkasa huo.