VIDEO: Soko kuu Kariakoo linawaka moto

VIDEO:Soko kuu Kariakoo linawaka moto

Muktasari:

  • Soko Kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam linaungua moto usiku huu huku jitihada za kuuzima zikiendelea.

Dar es Salaam. Soko Kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam linaungua moto usiku huu huku jitihada za kuuzima zikiendelea.


Akizungumza na Mwananchi kwa simu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amethibitisha tukio hilo.


Makalla ambaye yuko kwenye eneo la tukio, amesema; “Ni kweli soko linaungua na tuko hapa tunapambana kuuzima moto”
Amesema moto huo umeanza kuwaka Saa 3:30  na chanzo bado hakijajulikana.


“Moto umeanza kama nusu saa iliyopita, tupo kwenye eneo tunapambana kuuzima” amesema Makalla ambaye hakutaja chanzo cha moto huo.
 
Endelea kufuatilia Mwananchi kwa habari zaidi