Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Watatu wafariki kwa kufukiwa na kifusi Sikonge

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Richard Abwao

Muktasari:

Watu watatu wamefariki dunia baada ya kufukiwa na kifusi katika Kijiji cha Misheni wilayani Sikonge.

Tabora.  Watu watatu wamefariki dunia baada ya kufukiwa na kifusi katika Kijiji cha Misheni wilayani Sikonge.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Richard Abwao amesema watu hao walifariki jana Jumanne Novemba 16, 2021 wakati wakati wakichimba mchanga.

"Chanzo ni kuporomoka kwa kifusi au udongo na kuwaangukia wakati wakiwa chini wanachimba udongo" amesema.

Kamanda Abwao ameeleza kuwa shimo lililosababisha vifo ni mabaki ya mojawapo wa mashimo yaliyochimbwa katika ujenzi barabara.

Amewataja waliofariki kuwa ni Bakari Shaban (21), Sadick Ramadhan (9) na Rashid Hamis (9) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tatu Katika Shule ya Msingi Majengo.

Kamanda Abwao amewataka wananchi kuwa waangalifu wanapochimba udongo katika mashimo.