Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Zimamoto wazindua namba mpya ya dharura

Muktasari:

Kabla ya kuzinduliwa kwa namba hiyo mpya, watu walilazimika kuripoti majanga ya moto kupitia namba za dharura za polisi

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji nchini, likishiriakiana na asasi ya kiraia iitwayo United Against Crime, wamezindua kampeni ya kuitangaza namba mpya - 114 - ya dharura kwa ajili ya kupiga pindi yanapotokea majanga mbalimbali yakiwamo ya moto.

Uzinduzi huo umefanyika leo Jumanne Agosti Mosi makao makuu ya jeshi hilo jijini Dar es Salaam na umekwenda sanjari na kuhamasisha Watanzania kufahamu kwa undani majanga ya moto na namna ya kukabiliana nayo

Kamishana Jenerali wa jeshi hilo, Thobias Andengenye, amewaambia wanahabari kuwa namba hizo zitawasaidia Watanzania kupiga simu na kupatiwa huduma za uokozi haraka.

"Watu wengi wanaifahamu namba 112 ambayo ni polisi lakini 114 hawaifahamu vizuri, hali inayosababisha kutumia muda mwingi kupiga 112 badala  ya 114. Nina imani sasa hivi watakuwa wanaitumia  namba hii," anasema Kamishna Andengenye.

Amesema uzinduzi huo wa kampeni unakwenda sambamba na mchakato wa kuwajengea uewela Watanzania wa namna ya hatua za kuchukua na kukabiliana na majanga ya moto

Katibu Mtendaji wa United Against Crime, Andrew Elliot amesema wameamua kuweka nguvu katika kampeni ili kuokoa Watanzania na majanga ya moto na kwamba kupitia mchakato huo Watanzania watajengewa uwezo mkubwa wa kukabiliana na majanga hayo.

Elliot amesema katika kampeni hiyo wamesharikiana na watu mbalimbali ikiwamo kampuni ya Mabati ya Alfa na Selc