Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Lima vitunguu kisasa-6

Muktasari:

  • Hili ni banda lenye uwazi mkubwa, lenye upana usiozidi mita tano, na urefu toka chini hadi juu usizidi mita mbili na nusu.

Nukta ya makala iliyopita ilikuwa uhifadhi wa vitunguu baada ya kuvuna. Endelea

Hifadhi kwa kuninginiza vitunguu kwenye banda

Hili ni banda lenye uwazi mkubwa, lenye upana usiozidi mita tano, na urefu toka chini hadi juu usizidi mita mbili na nusu.

Banda linajengwa kwa miti, fito, mbao au mianzi na vitunguu vinahifadhiwa kwa kuninginiza kwenye fremu za fito ndani ya banda. Safu za vitunguu hupangwa kufuata urefu wa banda na kimo cha banda.

Urefu wa banda huelekezwa kwenye mkondo wa upepo ili kuruhusu upepo kuingia na kutoka. Banda liezekwe kwa nyasi ili kudhibiti joto na jua. Kribu au banda vinahifadhi vitunguu vizuri kwa muda wa miezi sita bila kuharibika.

Upotevu wa vitunguu ghalani

Vitunguu vingi hupotea wakati wa kuhifadhi kwa sababu ya kuoza, kuota (toa majani na mizizi) na kupoteza uzito

Kuoza

Kuoza kwa vitunguu vikiwa ghalani kunasababishwa na vimeliea vya fangasi au bakteria. Joto pamoja na unyevunyevu ndani ya ghala, husababisha kuzaliana na kuongezeka kwa vimelea vya magonjwa.

Kudhibiti: Weka ghala katika hali ya usafi, kausha vizuri na chambua vitunguu kabla ya kuhifadhi.

Muozo kitako

Vimelea vya aina ya fungus vinavyoishi kwenye udongo, vinashambulia sehemu ya chini ya vitunguu. Vimelea vinapenya kwenye sehemu zenye michubuko inayotokea wakati wa palizi, kuvuna au kusafirishwa. Vitunguu vinaoza na baadaye vinakauka na kusinyaa.

Njia zifuatazo zinadhibiti: mzunguko wa mazao, uchambuaji mzuri kabla ya kuhifadhi na

kuepuka michubuko wakati wa palizi na kuvuna

b) Ukungu mweusi (Black mould)

Ugonjwa huu unaletwa na vimelea vya fangasi vinavyoishi kwenye udongo. Vimelea vinazaliana katikati ya maganda na ukungu mweusi kama poda unaonekana. Baadaye maganda yanasinyaa na kuvunjika.

Kudhibiti

•Kutumia mzunguko wa mazao

•Kukagua ghala mara kwa mara na kuondoa vitunguu vilivyooza

•Kuweka ghala katika hali ya usafi.

•Kuondoa masalia ya vitunguu na kuchoma moto.

c) Kuoza shingo (Neck rot)

Vimelea vya fangasi vinashambulia vitunguu vikiwa shambani kabla ya kuvuna. Ugonjwa hauonekani mpaka vitunguu vikomae, vivunwe, vikaushwe na kuhifadhiwa ghalani, ndipo ugonjwa hujitokeza.

Ugonjwa unasababisha kuoza kwa vitunguu. Maganda ya vitunguu yanalainika kuanzia shingoni na nyama ya kitunguu huwa na sura ya maji maji. Vitunguu vilivyooza vinanyauka na kusinyaa.

Kudhibiti: kausha vitunguu vizuri kabla ya kuhifadhi, choma na kuharibu masalia ya vitunguu shambani na ghalani.

d) Muozo laini

Ugonjwa unasababishwa na vimelea vya bakteria. Dalili kubwa ya ugonjwa huu ni kulainika kwa vitunguu na kutoa harufu mbaya. Ukiminya kitunguu maji yenye harufu mbaya yanatoka kwenye shingo.

Muozo laini unatokea wakati hali ya hewa ikiwa na unyevunyevu na joto. Pia vitunguu vyenye shingo nene ambavyo havijakauka vizuri ni sehemu nzuri sana ya vimelea kuzaliana.

Makala haya yameandaliwa na Mogriculture 0655-570-084. www.mogriculture.com