Barbara afunguka mtandaoni

Katika hali ambayo haijafahamika, Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez amefunguka leo kupitia ukurasa wake wa Twitter akisisitiza msamaha.


Barbara ameandika ujumbe mfupi wenye maneno tisa kwa Kingereza unaolenga kutafuta au kutuliza amani.


Mtendaji huyo ameandika, “When you have a chance to seek revenge: FORGIVE! (Ukipata nafasi ya kulipiza kisasi, samehe),”
Barbara ameandika ujumbe huo muda mfupi kabla ya aliyekuwa Msemaji wa Simba, Haji Manara kutema nyongo tangu aondolewe kwenye nafasi hiyo.