Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Salah aweka rekodi Liverpool ikiifuata PSG robo fainali Ulaya

Mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah amefikisha idadi ya mabao 50 katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Picha na Mtandao

Muktasari:

  • Salah amefikisha idadi ya mabao 50 katika Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa mchezaji wa kwanza kutoka Afrika kufikia idadi hiyo.

Liverpool, England. Liverpool wameonesha kiwango cha juu na kuifunga Galatasaray mabao 4-0 yaliyoifanya timu hiyo kufuzu hatua robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa jumla ya mabao 4-1 ambapo watakutana na mabingwa watetezi, Paris Saint-Germain (PSG)

Baada ya kupoteza 1-0 jijini Istanbul wiki iliyopita, kikosi cha Arne Slot kilisawazisha matokeo ya jumla wakati Dominik Szoboszlai alipofunga bao kufuatia mpira wa adhabu.

Kabla ya mapumziko, Mohamed Salah alikosa penalti baada ya kipa, Ugurcan Cakir kuokoa, lakini Liverpool walifunga mabao matatu ndani ya dakika 11 za kipindi cha pili na kumaliza kabisa mchezo huo.

Hugo Ekitike alifunga bao la karibu baada ya pasi nzuri kutoka kwa Salah, kisha Ryan Gravenberch akafunga baada ya shuti la Salah kuokolewa na Cakir.

Wilfried Singo aliujaza mpira wavuni kwake mwenyewe kufuatia krosi ya Jeremie Frimpong, lakini bao hilo lilikataliwa kwa sababu Frimpong alikuwa ameotea. Dakika chache baadaye, Salah alipachika bao zuri sana.

Akiwa nje ya eneo la hatari, Salah alipiga shuti la kona kali lililoingia moja kwa moja juu ya lango, mtindo wake wa kawaida na kufikia mabao 50 ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, hivyo kuwa mchezaji wa kwanza kutoka Afrika kufikia idadi hiyo.

Liverpool wangeweza kufunga mabao zaidi, huku Salah akipiga mpira uliogonga mwamba na pia kipa Cakir akiokoa mara kadhaa.

Galatasaray hawakuwa na mashabiki wao uwanjani Anfield kutokana na adhabu ya UEFA kufuatia vurugu zilizotokea katika mechi yao ya awali ya ugenini dhidi ya Juventus.

Matokeo hayo yanaifanya England kuwa na timu mbili katika robo fainali, baada ya Manchester City, Chelsea, Newcastle na Tottenham kutolewa, huku Arsenal wakitarajiwa kukutana na Sporting katika robo fainali nyingine.

Kwa Arne Slot, hii ni mara yake ya kwanza kufika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, na atapata nafasi ya kulipiza kisasi dhidi ya kikosi cha Luis Enrique ambacho kiliiondoa Liverpool msimu uliopita.