Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Puma Energy yatwaa tuzo mbili kubwa za heshima wiki moja

Dar es Salaam. Kampuni ya Puma Energy Tanzania imejizolea tuzo mbili kubwa za heshima ndani ya wiki moja, hatua inayoendelea kuimarisha nafasi yake kama mchezaji muhimu katika sekta ya nishati na usambazaji nchini.

Tuzo hizo zimetolewa kupitia programu za CSW Tanzania Events zinazolenga kutambua ubora, ufanisi na ubunifu katika sekta za usafirishaji, nishati na biashara.

Katika tuzo ya kwanza, Puma Energy Tanzania ilitangazwa kuwa Kampuni Bora ya Usambazaji wa Mafuta na Nishati ya Mwaka katika Africa Transportation Excellence Awards Night 2026, iliyofanyika katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam. Tuzo hiyo imeitambua kampuni kwa mchango wake katika usambazaji wa mafuta, ubunifu wa suluhisho za nishati na kuimarisha ufanisi na uaminifu katika mnyororo wa usafirishaji.

Katika tuzo ya pili, kampuni hiyo ilipokea Tuzo ya Heshima kama Kampuni Bora ya Biashara, Usambazaji na Suluhisho za Kibiashara katika General Trading Business Networking Gala, iliyofanyika pia Dar es Salaam. Tuzo hiyo imetolewa kuenzi utendaji bora katika biashara ya usambazaji, ufanisi wa mnyororo wa ugavi na mchango wake katika sekta ya mafuta na gesi.

Puma Energy Tanzania imepongezwa kwa ubora wa huduma, ufanisi wa kiutendaji na mchango wake katika kuimarisha sekta ya nishati na biashara nchini.

Tuzo hizo mbili zinaendelea kuipa kampuni hiyo nafasi ya kuonekana kama mshirika wa kuaminika, huku ikisisitiza dhamira yake ya kuleta ubunifu, ufanisi na ukuaji endelevu katika sekta ya nishati.