Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Bashe: Hakuna nzige Tanzania

Muktasari:

Naibu Waziri wa Kilimo nchini Tanzania, Hussein Bashe amesema hakuna nzige walioingia Tanzania kama inavyodaiwa.

Dodoma.  Naibu Waziri wa Kilimo nchini Tanzania, Hussein Bashe amesema hakuna nzige walioingia Tanzania kama inavyodaiwa.

Amesema ikiwa wataonekana nchini watashughulikiwa kabla ya kuleta madhara kwa wakulima.

Ametoa kauli hiyo leo Alhamisi Februari 13, 2020  wakati  akizungumza na wadau wa kilimo, mifugo na uvuvi katika kongamano  lililofanyika mkoani Dodoma.

Nzige walionekana kwa wingi nchini Kenya na hivi karibuni mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira amesema walionekana mkoani humo, baadaye kutoweka kusikojulikana.

Amesema baada ya taarifa za nzige kuwa wamesogea katika ardhi ya Tanzania, Serikali ikipeleka wataalamu mipakani kwa ajili ya kufanya uchunguzi na taarifa inaonyesha hadi leo hakuna mahali walipoonekana

"Tumechukua hatua za kutosha kuhakikisha wanaoonekana katika ardhi yetu wanashughulikiwa kikamilifu bila kuleta madhara kwa wakulima wetu," amesema.