Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Maajabu, ziara ya IShowSpeed Afrika 

Muktasari:

  • Kupitia safari zake katika baadhi ya nchi za Afrika, IShowSpeed amefanikiwa kuvuta hizia za mamilioni ya watu duniani wanaofuatilia live streams zake Afrika

Dar es Salaam. Ziara ya Africa inayofanywa na staa wa mitandao ya kijamii duniani kutokea Marekani, Darren Watkins Jr maarufu IShowSpeed, imeendelea kuacha alama kubwa katika sekta ya burudani, utalii na mitazamo dhidi ya Waafrika.

Kupitia safari zake katika baadhi ya nchi za Afrika, IShowSpeed amefanikiwa kuvuta hizia za mamilioni ya watu duniani wanaofuatilia live streams zake Afrika.

Maajabu yaliyojitokeza kwenye ziara yake ni kuwa baadhi watu Ulaya, walikuwa wanadhani Afrika ni bara linalokabiliwa na umaskini, migogoro na watu wasio staarabika. Lakini ziara hiyo imebadili mitazamo hiyo hasi kwa kiwango kikubwa.

Kupitia video zake, ameonesha Afrika kuwa na vijana wachangamfu, tamaduni, muziki wa kuvutia, chakula cha asili na mazingira mazuri. Hili limechangia kuongeza hamasa ya utalii na kuwafanya vijana wengi wa kimataifa kutamani kutembelea Afrika. 

Hili linathibitika katika baadhi ya video na komenti zinazotolewa na watu kutoka mataifa ya nje ya Afrika wakieleza mitazamo yao ya awali ilivyokuwa hasi kuhusu Afrika, huku wengine wakidai hawakuwahi kufahamu kuwa Afrika kuna barabara, maji safi, umeme, majengo makubwa na hata watu wastaarabu.

IShowSpeed ni nani?

Ni mmoja wa watu maarufu zaidi kwenye mitandao ya kijamii duniani, hususan kupitia  YouTube ambako ana  wafuasi 48.2 milioni, Instagram 43.7 milioni na Tiktok ni 46.1 milioni. 

Alizaliwa Januari 21, 2005 nchini Marekani, alianza kujulikana kwa kasi kutokana na video zake za live akicheza games, burudani, muziki na vichekesho. IShowSpeed pia ni msanii wa muziki, akiwa na nyimbo kadhaa zilizopata umaarufu mtandaoni. Hadi sasa tayari ametembelea  Angola, South Africa (Afrika Kusini), Mozambique , Eswatini, Botswana, Zimbabwe, Zambia, Rwanda na Kenya