Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Bashe aagiza kuundwa timu huru kuchunguza bei ya korosho

Muktasari:

  • Kufuatia kuwapo sintofahamu kadhaa kwenye zao la korosho ikiwamo bei, Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe ameagiza kuundwa  timu huru ya kuchunguza changamoto za zao hilo msimu huu, ambayo itafanya kazi ndani ya siku 14.

Mtwara. Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe ameagiza kuundwa timu huru ya kuchunguza changamoto za zao la korosho zilizojitokeza katika msimu huu.

Malalamiko yaliyogubika zao hilo msimu huu ni  soko la awali linalotajwa kuangusha bei ya korosho, zao hilo linapitishwa kwenye Bandari ya Mtwara bila kupimwa na kuwapo na madhara ya kusafirisha bidhaa hiyo usiku.

Agizo hilo lilitolewa na Bashe Novemba 27,2023  kwa kupiga simu kwenye kikao kilichokuwa kikiendelea kikihusisha  vyama vikuu, waendesha maghala, warajis na wadau wengine wa korosho kutoka katika mikoa mitatu inayolima zao hilo kilichokuwa kinajadili  mauzo ya korosho ghafi. Kwa maelezo ya kiongozi huyo alipiga simu baada ya  kuona malalamiko hayo kwenye mitandao.

Amesema kuwa ameziona hoja tatu zilizotolewa na Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha MAMCU, Siraj Mtenguka zikiwamo soko  la awali kuangusha  bei ya korosho, Bandari ya Mtwara korosho zinapita bila kupimwa na  kusafirisha korosho usiku kunaleta madhara.

“Kutokana na madai hayo Mwenyekiti huyo aliomba  kuundwa timu ya uchunguzi, sawa naagiza hiyo timu huru iundwe na mwenyekiti wa MAMCU awemo ili tuone kama hayo malala,iko  ndiyo yanasababisha kuanguka kwa bei ya korosho,”amesema Bashe.

Ametaja wanaopaswa kuwepo ndani ya timu hiyo kuwa ni Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), watu wawili kutoka wizarani, mwenyekiti wa Mamcu, huku akiwaagiza mbali  ya kuangalia mambo hayo  matatu pia waangalie suala la kulaza nje debe kama kunasababisha changamoto kwenye soko.

“Hii timu naipa siku 14 tu wakachunguze soko la awali, korosho zinazopita bila kupimwa Bandari ya Mtwara, madhara ya kusafirisha korosho usiku  je, kunaleta madhara kama ya wizi ama kuchanganya na zenye ubora hafifu, kulaza debe kama kunaathiri bei sokoni. Wizarani nitamwambia katibu mkuu alete watu wawili,” amesema Bashe.

Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Masasi & Mtwara Cooperative Union (MAMCU), Silaj Mtenguka amesema, “Sisi tulishasema kuwa hatuliziki na utaratibu wa soko la awali na tulikuwa na mwongozo , lakini tumeletewa mwingine tena katikati ya msimu bila wadau kushirikishwa na ndio unasema tusafirishe korosho usiku.

“Mnada wa kwanza wanunuzi 42, mnada wa pili wanunuzi 50 baadaye wakashuka zaidi huu mwongozo ulibadilisha ambapo wanunuzi walipungua wakafika 20 tukajiuliza kwa nini? kumbe wale wanunuzi waliotoka nje ya nchi ndio wananunua korosho kupitia soko la awali hii ni kama kangomba iliyochangamka.

“Soko la awali limetushushia bei ya korosho haiwezekani mnunuzi amekuja Tanzania ananunua kwa wakulima korosho kwa Sh1300-1500 hata akienda mnadani hawezi kupandisha bei huku anapewa nafasi ya kusafirisha korosho usiku,” amesema na kuongeza.

“Hatujiulizi kwa nini mzani wa bandarini ulibadilishwa na umeanza kutumika jana kuna nini wakati korosho ikitoka ghala kuu inatakiwa kuhakikiwa sasa pasipo mzani tunahakikishaje,” amesema Mtenguka.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Francis Alfred amesema kuwa kikao hicho ni maalumu kwa ajili ya kufanya tathmini na mweneno wa soko la korosho ghafi unaonekana kushuka.