Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Anayedaiwa kuzini na mwanaye afikishwa mahakamani

Anayedaiwa kuzini na mwanaye afikishwa mahakamani

Muktasari:

  • Ikwabe Gibogo (58) aliyekamatwa kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wake mwenye umri wa miaka 11 amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi  Wilaya ya Serengeti.

Serengeti. Ikwabe Gibogo (58) aliyekamatwa kwa tuhuma za kumlawiti mtoto wake mwenye umri wa miaka 11 amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi  Wilaya ya Serengeti.

Akisoma mashtaka leo Jumanne Januari 26, 2021 mbele ya hakimu Adelina Mzalifu, mwendesha mashtaka  wa Serikali, Paskael Nkenyenge  amesema mshtakiwa huyo wa  kesi hiyo namba 9 ya mwaka 2021 anakabiliwa na shtaka la kuzini na maharimu.

Amebainisha kuwa Januari 23, 2021 eneo la Chamoto, mtuhumiwa alikamatwa kwa kosa la kuzini na mwanaye  kinyume na kifungu namba 158 (1)(a)  cha kanuni ya adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2019.

Gibogo alikana mashtaka na kupelekwa mahabusu kesi hiyo ikiahirishwa hadi Februari 9, 2021.