Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Jinsi TADB inavyo chochea Taifa kuwa na utoshelevu wa chakula

Muktasari:

  • Ripoti ya Shirika la kima­taifa la chakula na kilimo (FAO, 2018) inabainisha kuwa ifikapo mwaka 2050, ziada ya asilimia 60 ya chakula itahitajika ili kukidhi mahitaji ya watu. Inakadiri­wa kuwa ifikapo mwaka 2050 dunia itakuwa na watu wapatao bilioni 9.8.

Ripoti ya Shirika la kima­taifa la chakula na kilimo (FAO, 2018) inabainisha kuwa ifikapo mwaka 2050, ziada ya asilimia 60 ya chakula itahitajika ili kukidhi mahitaji ya watu. Inakadiri­wa kuwa ifikapo mwaka 2050 dunia itakuwa na watu wapatao bilioni 9.8.

Kwa ongezeko hili la watu duniani, kwa pamoja mataifa yanatahadharishwa kuchu­kua hatua madhubuti katika kuhakikisha kwa pamoja janga la njaa linatokomezwa, kuhakikishaongezeko la uza­lishaji wa mazao ya chaku­la, kupunguza upotevu wa chakula na kuwa na utoshe­levu na usalama wa chakula.

Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ni moja ya taasisi muhimu nchini katika kuwezesha mafanikio ya jitihada za Taifa katika kuwezesha nchi kuwa na uhakika na usalama wa chakula. Kwa kutambua uhitaji wa mitaji katika kuon­geza uzalishaji wa mazao ya Kilimo, TADB ilianzishwa kama chombo kitakacho chagiza upatikanaji wa mit­aji na kuwa chachu katika kufikia mapinduzi ya kilimo.

“Kwa kuzingatia dhana ya uwepo wa benki yetu ya maendeleo ya kilimo Tan­zania, waasisi walitambua umuhimu wa kuchagiza mapinduzi katika kilimo, uvuvi na mifugo kwa kuan­za na kuangalia upatikanaji wa mitaji katika kuzalisha mazao ya chakula. Sekta hizi ni muhimu katika juhudi za nchi kuwa na uhakika wa chakula. Hivyo, kama taasisi, tumekuwa na njia mbalim­bali za kuwezesha nchi yetu kuwa na uhakika wa chaku­la,” anasema Mkurugenzi Mtendaji wa TADB, Frank Nyabundege.

Kupitia ripoti na tafiti mbambali ambazo TADB imezifanyia kazi, baadhi ya mambo yanayobainishwa kama changamoto katika kuwezesha Taifa kuwa na uhakika wa chakula ni pamo­ja na; kasi ya ongezeko la watu, upatikanaji wa mitaji, matumizi hafifu ya kilimo cha umwagiliaji na kutokuwa na matumizi ya teknolojia sahihi katika kilimo. Chan­gamoto nyingine ni pamoja na; ubora wa mbegu, upati­kanaji wa pembejeo na upo­tevu wa mazao.

Uwezeshaji mitaji katika sekta ya chakula.

Zaidi ya asilimia 35 ya Sh99.4 bilioni ya mikopo ya TADB imeelekezwa moja kwa moja kwenye minyoro­ro ya thamani ya mazao ya chakula. Ambapo asilimia zaidi ya asilimia 8 imeele­kezwa katika pembejeo kama vile mbegu bora, mbo­lea na viwatilifu.

“Matumizi ya mbegu bora katika kilimo ni jambo muhimu sana. Hata kuwa na mbegu bora ya ng’ombe, kuku au mbuzi ni jambo linalochagiza ongezeko la chakula nchini,” anasema Nyabundege.

Pamoja na kuwezesha mitaji miongoni mwa waku­lima na miradi ya kilimo cha mazao ya chakula, TADB pia imeshirikiana na taasisi mbalimbali kama Wakala wa Mbegu (ASA), Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI) n.k ili kuchochea kuongeza uza­lishaji wa mbegu bora. Kwa ushirikiano kama huu TADB inasaidia ongezeko la upati­kanaji wa mbegu bora kwa wakulima chini.

Kilimo cha umwagiliaji

TADB imeweze­sha zaidi ya Sh9 bilioni katika kuweze­sha kilimo cha umwagili­aji. Mabadiliko ya tabia nchi yameathiri kiwango cha upatikanaji wa mvua na kubadili muundo uliozoeleka wa hali ya hewa. Kumekua na baadhi ya mae­neo yakikabiliwa na vipindi virefu zaidi vya jua na hivyo kupelekea ukame, baadhi ya maeneo yakipata mvua chache zaidi, na mengine kupata mvua nyingi zaidi ya inayohitajika. Mabadiliko haya yamechangia kupun­guza mavuno ya mazao ya chakula katika baadhi ya maeneo.

“TADB imeona fursa ya kuwezesha wakulima kuen­delea kuzalisha pasi kutege­mea mvua kwa kuwezesha miun­dom­binu inayowezesha kilimo cha umwagiliaji. Kwa kuboresha miundombinu hii tumeweza kuwa na uhakika wa mazao kama ya mpunga yanayo­zalishwa kwenye skimu za umwagiliaji kama vile skimu ya umwagiliaji Mombo, chama cha wakulima na Umwagiliaji Ruvu (CHAURU) ambapo zaidi ya wakulima wadogo 1,500 wanalizalisha mpunga,” anasema Nyabun­dege.

Uhifadhi na uchakataji wa mazao ya chakula

Wakati Taifa likijizatiti kuwa na uhakika wa chaku­la, upotevu wa mazao nao unabainishwa kuwa moja ya changa­moto katika kufikia lengo hilo. Upo­tevu wa mazao ya chaku­la huchan­gia upungufu wa mavuno na kupunguza ubora wa mazao na virutubisho katika mazao. Ripoti ya shirika la kimataifa la IITA inaonesha kuwa Tanzania hupoteza asilimia 25 ya mazao waka­ti wa mavuno na kupoteza asilimia 15 ya mavuno kwa kutokuwa na uhifadhi bora.

Kwa kutambua haya, TADB imewezesha jumla ya Sh 3 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa maghala yenye uwezo wa kuhifadhi mazao zaidi ya tani 50,000. Pamoja na kujenga maghala ya kuhifadhi chaku­la, benki imewezesha zaidi ya Sh100 bilioni iliyokwenda katika viwanda vya kuchaka­ta mazao mbalimbali kama vile mahindi, maziwa, nya­ma na samaki.

“Kupitia mfu­mo wa kuunganisha wadau muhimu katika mnyororo wa thamani (IVCF model) TADB imewaunganisha wakulima wadogo na wachakataji wa mazao ilikuhakikishia wa zalishaji masoko na pia kupunguza upotevu wa mazao kutokana na kuharibika wakati wa kuhi­fadhi.

Kwa kuongeza tha­mani ya mazao ya chakula tunawezesha chakula kuhi­fadhiwa kwa ubora zaidi na hivyo kufaa kwa matumizi ya muda mrefu,” anasema Nyabundege.

Zana bora za kisasa

Kama ilivyo muhimu kuwa na simu ya kiganjani katika zama hizi za kidigitali, ndi­vyo ilivyo pia muhimu kutumia zana bora za kilimo kwa kilimo chenye tija. Matumizi sahihi na zana sahihi za kili­mo ni moja ya njia inayocho­chea kuongeza tija katika mazao ya chakula.

Tanzania ina jumla ya hekta millioni 44 zinazofaa kwa kilimo huku asilimia 33 tu ya eneo hilo ikitumika kwa sasa. Kwa kuwezesha upatikanaji wa zana bora za kisasa, tutaweza kucha­giza ongezeko la uzalishaji wa mazao ya chakula hivyo kuwezesha Taifa kuwa na utoshelevu wa chakula.

Akifafanua zaidi, Nyabun­dege anasema TADB imewezesha jumla ya Sh5.9 bilioni ambapo waku­lima wameweza kupata trekta na mashine za kuvu­nia mazao ya nafaka kama vile mpunga. Katika sekta ya uvuvi pia wamewezesha ufu­gaji wa vizimba katika Ziwa Victoria na boti za uvuvi.

Pamoja na kuchangia jiti­hada za kuweza kuwezesha taifa kuwa na utoshelevu wa chakula nchini, TADB imeen­delea kujikita katika kuweze­sha ongezeko la uzalishaji, kuongeza thamani, uchakat­aji na uhifadhi wa mazao ya mifugo, uvuvi na kilimo.

“Mfano katika sekta ya uvuvi na mifugo, TADB imewezesha upatikanaji wa mfumo baridi (cold chains) ili kuhakikisha ubora na usalama wa mazao yatokanayo na uvuvi. Tumewezesha zaidi ya Sh2.2 bilioni kwenye sekta ya uvuvi na Sh9 bilioni kwenye sekta ya mifugo,” anasema Nyabundege.

Zaidi ya asilimia 80 ya chakula nchini huzalishwa na wakulima wadogo. Kwa kuzingatia hilo, TADB kupi­tia mfuko wake wa dhama­na kwa wakulima wadogo (SCGS) imewezesha jumla ya Sh57.5 bilioni ambapo zaidi ya wakulima wadogo 3,962 wamenufaika.

TADB inatambua umuhimu na kuamini katika ushirikiano katika juhudi za kuwezesha Taifa kuwa na utoshelevu wa chakula. Hivyo kuendelea kushiriki­ana na wadau mbalimbali katika kuleta mapinduzi hal­isi na yenye tija katika sekta ya Kilimo, Uvuvi na Mifugo.

“Kwa pamoja tutaweza kutengeneza mazingira bora kwa ajili ya uzalishaji wenye tija na mavuno bora kwa lishe na maisha ya watanza­nia,” anasema Nyabundege.