Kesi ya kina Mbowe yaahirishwa, washinda pingamizi

Muktasari:

Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi imeahirisha kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu.

Dar es Salaam. Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi imeahirisha kesi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na wenzake watatu.

Jaji Joachim Tiganga anayesikiliza ameahirisha kesi hiyo mpaka kesho Jumanne Januari 11, 2021 saa tatu asubuhi baada ya shahidi wake wa nane, Mkuu wa Upelelezi wa Polisi Wilaya (OC-CID) Arumeru, Mrakibu wa Polisi (SP), Jumanne Malangahe kumaliza ushahidi na upande wa utetezi kuanza kumhoji shahidi huyo.

Wakati mawakili hao wakiendelea na kumhoji shahidi, Wakili wa utetezi Peter Kibatala aliiomba mahakama iahirishe kesi hiyo mpaka kesho akidai kuwa bado ana maswali mengi lakini muda umepita, hoja ambayo iliridhiwa na pande zote na kumfanya Jaji Tiganga kuahirisha kesi hiyo.

Mapema asubuhi kesi hiyo ambaypo ilisimama kwa siku 21 kupisha mapumziko ya sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya 2022 ilianza kwa Jaji kutoa uamuzi mdogo wa pingamizi lililokuwa limewekwa na upande wa utetezi.

Akitoa uamuzi huo mdogo, Jaji Tiganga aliridhia Mahakama kutokupokea sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kama moja ya kielelezo ambapo upande wa utetezi ulidai kuwa kielelezo hicho kipo kinyume na sheria.

Baada ya uamuzi huo, Mahakama iliendelea na usikilizaji wa ushahidi wa shahidi wa nane wa upande wa mashtaka ambaye ni Mkuu wa Upelelezi wa Polisi Wilaya (OC-CID) Arumeru, Mrakibu wa Polisi (SP), Jumanne Malangahe.


Hapa ni mwanzo mwisho wa muenendo wa kesi hiyo ilivyoendelea leo


Jaji Joachim Tiganga ameshaingia mahakamani kwa ajili ya kusoma uamuzi

Mawakili wa pande zote wameanza kujitambulisha.

Jaji Tiganga anawaita majina washtakiwa mmoja baada ya mwingine

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji shauri linakuja kwa ajili ya kupokea uamuzi na kuendelea na ushahidi

Jaji: Upande wa utetezi?

Kibataka: Mheshimiwa Jaji nasisi tupo tayari kupokea uamuzi na kuendelea na kesi


Jaji: Nilitoa maelekezo hapa mahakamani, mtu yoyote anayeingia amwe amevaa maski (barakoa) kwanini wengine hawajavaa??

Jaji: Nina excuse ya wakili mmoja ambaye havai ...sasa wengine je?

Wakili Mallya: Mimi nina tatizo kidogo lakini nimechukua tahadhari zote za kujikinga na Uviko-19.

Baada ya Maelezo hayo, mmoja wa wafuasi wa Chadema alitoka nje na kwenda kuvaa barakoa kisha kuingia ndani huku watu wengine waliokuwepo ndani ya mahakama waliokuwa wameshusha barakoa zao chini ya pua,  wakizipandisha barakoa zao juu ya pua

Jaji Tiganga ameanza kusoma uamuzi wa kesi ndogo ndani ya kesi ya msingi.


Jaji Tiganga: Upande wa utetezi wao walianza na hoja moja kuwa kielelezo hicho namba 14 (Hati ya ukamataji mali) kilichezewa hivyo wanaomba ihesabike kuwa kisipokelewe na mahakama kwa sababu hajikidhi vigezo.

Jaji Tiganga: Kwa upande wa mashtaka wao walijibu hoja za upande wa utetezi kwa kueleza kuwa upande wa utetezi wametafsiri vibaya tafsiri ya sheria na kusema suala la utunzaji wa vielelezo linafahamika  na upande wa mashtaka haulazimishwi kutoa vielelezo vyote.

Jaji Tiganga: Upande wa mashtaka wakaendelea kuomba korti ipokee kielelezo hicho kwa sababu kimekidhi vigezo.

Jaji: Upande wa mashtaka uliendelea kueleza kuwa shahidi wa nane wa upande wa mashtaka SP Jumanne Malangahe aliandika maelezo namna alivyomtambua shahidi na namna alivyowasilisha vielelezo hivyo kwa mtunza vielelezo aitwaye Sajenti Johnstone.

Hivyo upande wa mashtaka waliomba mahakama ipokee kielelezo hicho kwa sababu hakikuchezewa na kilifuata mnyororo wa utunzaji.

Upande wa mashtaka waliendelea kuiomba mahakama ipokee kielelezo hicho baada ya kupitia mnyororo wa utunzaji wa kielelezo.

 Jaji: Pia upande wa mashtaka walieleza kuwa shahidi wa nane SP Jumanne Malangahe ndio aliyevikamata vielelezo hivyo na ndio yeye aliyevitoa mahakamani baada ya kuvitoa kwa mtunza vielelezo.

Jaji: Upande wa utetezi wakiwasilisha nyongeza yao ya kuwapinga vielelezo hivyo walieleza kuwa shahidi alitakiwa aviandike vielelezo hivyo katika notebook yake ili kuepuka vielelezo visichezewa.

Jaji: Hoja kuhusu Competent iliyotolewa na upande wa utetezi kuhusu kielelezo hicho kwamba hakukuwa na uthibitisho uliotolewa kama kweli sare hizo ninmali ya JWTZ

Jaji- Wakili Mallya alidai kuwa vielelezo hivyo ni vya kijeshi na nilitakiwa kutolewa kwa majina ya kijeshi.

Mallya alidai mfano kuna kielelezo shahidi alikita kuwa ni koti la mvua au ponjoo wakati kwa lugha ya kijeshi linatambulika kama sleeping bag.

Jaji: Wakili Mallya aliendelea kueleza kuwa kwa mazingira hayo shahidi huyo SP Jumanne Malangahe hana uelewa wa kutosha kuhusiana na vielelezo vyenyewe, hivyo wanaomba vielelezo hivyo visipokelewe.

Mallya aliendelea kueleza kuwa shahidi wa nane huyo hajaithibitishia wala hakuleta ushahidi wake mahakakani kama ni mtaalamu wa utambuzi wa vifaa vya kijeshi

Jaji: Kwa upande wa mashtaka kupitia wakili Kidando akijibu hoja ya wakili Mallya alidai kuwa shahidi alitambua vielelezo hivyo kwa alama alizoweka mwenyewe na kwamba sio lazima shahidi kuwa mtambuzi bali anatakiwa kuwa na ufahamu wa vifaa vya kijeshi.

Jaji: Hivyo upande wa mashtaka walidai maelezo aliyotoa Mallya kuwa vielelezo hivyo vimetolewa kwa majina tofauti havina mashiko kwa sababu Mallya yeye sio shahidi katika kesi hii, hivyo wanaomba Mahakama ipokee kielelezo hicho kwa sababu shahidi alitambua vielelezo hivyo kupitia alama alizoweka wakati wa ukamataji.

Jaji: kourti baada ya kupitia hoja za pande zote mbili zilizowasilishwa na Mallya, inatupilia mbali pingamizi hili.


Jaji: Kifungu pia cha 22(3) d  cha Sheria ya Uhujumu Uchumi inasema pia kuwa ni lazima kutoa risiti but pia PGO ya 226 (2,5) na yenyewe inasema kuhusiana na utolewaji wa risiti

Na mwisho Guidelines ya Mahakama Chapter 05 Paragraph ya 5 (f) inasema kuwa inatakiwa kutolewa risiti ya mali zilizokuwa zinakamatwa

Hakuna sehemu inayosema kuwa pale mahala ambapo risiti haijatolewa basi seizure Certificate itumie kama mbadala wa risiti

Kwa upande wa utetezi walikataa mwaliko huo kwa kuomba mahakama ikatae mwaliko huo kwamba risiti na seizure Certificate ni nyaraka mbili tofauti

Katika eneo hilo Mahakama inamaoni kuwa swala la risiti Mahakama imewekwa wazi na ni muhimu itumike

Suala la Certificate of Seizure (hati ya ukamataji) kutumika badala ya Risiti kuna Maamuzi ya mahakama ya Rufani ya ANDREA AGUSTINO na wenzake ikiwa imeamliwa huko Tanga katika Rufani ya Jinai.


Mahakama ilipo itwa Kuona Kuwa Risiti Itumike Mbadala wa Certificate of Seizure ilisema Kuwa

Basi ni wazi kuwa Mahakamani ya Rufani ilishaona kuwa jambo hili no vitu viwili tofauti na Mahakama inaona kuwa kutokutolewa kwa risiti Ni mambo mawili tofauti.

Baada ya kuwa tumeona kutokutolewa kwa risiti kuna athari, Mahakama ya Rufani Iliyoketi Iringa na Ilikuwa aime Quote with Approval katika Kesi ya PATRICK JEREMIAH Vs JAMHURI 34 / 2016

Kwa sababu hiyo Mahakama hii Inaona Kuwa Kushindwa Kutoa Kwa risiti ni Fatal na Jambo hili lina athiri Admissibility.



Kutokana na malekezo hayo ya Kisheria yakiyoelezwa katika PGO hiyo ni wazi kuwa alama iliyiwekwa siyo alama ambayo PGO 229 imeitambua na kuelekeza

Hata kama alama hiyo ingekuwa imevumiliwa basi kama ingekuwa alama hiyo iliwekwa mbele ya mashahidi hao basi ingevumilia

Hivyo, katika utaratibu huo Mahakama ina maoni kwamba alama hiyo iliyowekwa imekiuka PGO 229 kwa maana hiyo inaathiri afya ya kielelezo hicho na kuathiri Competence

Na nikitafuta matakwa ya Adminsibility kuwa Polisi ofisa alitakiwa kutoa risiti ya ku -acknowledge kukamata vielelezo hivyo

Hata hivyo jatika koja hiyo upande wa utetezi wanasema kuwa mtu yoyote ambaye anafanya upekuzi lazima atoe risiti baada ya upekuzi kama ambavyo Sheria inalekeza

Wanasema kuwa shahidi wa nane wa upande wa mashtaak hajasema kuwa ametoa risiti wala hajatoa nakala yoyote mahakamani kama alitoa risiti

Kwa namna hiyo wakialika sheria kwa kutokutoa risiti.

Katika majibu yake Wakili Kidando anasema kwa kufanya upekuzi na kukamata mali, Shahidi namba nane alitoa hati ya ukamataji mali ( Seizure Certificate).

Pia upende wa mashtaka wakasema kuwa kwa kutolewa Seizure Certificate ambayo ina content sawa na risiti wakaomba Mahakama wa one kuwa Seizure Certificate ionekane kama risiti

 Upande huo wa mashtaka waliendelea kwa kuomba Mahakama Izingatie Sehemu ya Pili katika sehemu A ya CPA, 2 (a) D Mahakama Ione kuwa Kuwepo Kwa Seizure Certificate ni sawa na Kutolewa Risiti


Hivyo, nakubaliana na upande wa utetezi kama ambavyo wameieleza Mahakama kuwa panapokuwa umefanyika upekuzi katika nyumba, box au eneo ofisa ambaye amekamatwa mali anatakiwa kutoa risiti juu ya mali alizokamata na nukuu Kifungu cha 38 (3)  ya CPA

Kifungu Kingine kinachohusika kutolewa na risiti ni kifungu cha 35(3) ya Sheria ya Polisi na Polisi Wasaidizi Sura ya 322


Uamuzi wa Jaji Tiganga: Katika hali ya kawaida Mahakama ilitakiwa kuishia hapa, lakini kuna mwaliko wa Kibatala kuwa Mahakama izingatie kuwa unatafuta nini kila inapokuwa Sheria inakiukwa lakini wanapewa nafasi upande wa mashtaka

Nimeona hakuna cha ku reconcile katika maamuzi ambayo nimeshayatoa, maamuzi yote niliyo yatoa ni maamuzi halali hivyo Mahakama inaona hoja hiyo halikuwa na mashiko na naitupilia mbali

Mahakama inaona hoja zote zilizoletwa na upande wa utetezi hayakuwa na mashiko isipokuwa mapingamizi mawili ya Lebelling na kutokutoa risiti

Na kwa mapingamizi haya Mahakama inaona yana merit na sababu nilizotoa mahakamani nakataaa vielelezo hivyo na ninatoa amri.

Jaji Tiganga baada ya kutoa uamuzi huo, Mawakili wa pande zote mbili wanakubaliana na uamuzi Jaji kwa kusimama na kumuinamia.

Jaji: Haya upande wa mashtaka tuanendela na ushahidi.







Baada ya Jaji kutoa uwamuzi shahidi wa nane anaendelea na ushahidi.

Jaji: Shahidi tunakukumbusha uko chini ya kiapo na utaendelea kutoa ushahidi wako.

Wakili Kidando anamuongoza Shahidi kuendelea na ushahidi.

Shahidi Jumanne Malangai Tarehe 24/2020 nikiwa Arusha nilifika eneo moja nililoliona kwenye mchoro linaitwa kilombero na kubaini ni soko lililoko katikati ya Jiji upande wa magharibi limepakana na gereza la kisongo, kutokea hapo umbali mfupi upande wa kulia kuna hilo soko la kilombero.

Nilipo endelea na upelelezi kesho yake tarehe 25, alikamatwa mtuhumiwa Elia Kaaya ambaye baadae aliachiwa baada ya upelelezi kukamailika

Justin Kaaya aliachiwa baada ya ushahidi kuonyesha alikuwa hausiki

Tuliendelea kufuatilia taarifa za watuhumiwa wengine ambapo tarehe 10/9 alikamatwa mtuhumiwa mwingine ambapo naebaliachiwa baadaa ya upelelezi kukamillika.

Mshtakiwa huyu kwa taarifa tulizopata alikuwa Miongoni mwa watuhumiwa waliokuwa washiriki kufanya uhalifu.

Tulifika mkoani Tabora na kukamata mtuhumiwa mwingine Gabriel Mhina tarehe 19/9/2020 nae alikuwa ni askari wa JWTZ Kikosi cha 92 KJ nae aliachiwa baada ya ushahidi kutokamilika

Kuna mtuhumiwa mwingine tulimkamata Mwanza tarehe 19 wakati tukiwa tunamfuatilia mtuhumiwa mwingine Malima ambaye nae aliwahi kuwa JWATZ Kikosi cha 92 KJ

Asubuhi nlitembelea eneo lingine Mwanza mjini ambapo kuna mkutano ya barabara kuelekea mabatini upande wa kushoto kuelekea benki ya BOT kuna kituo cha mafuta kinachoitwa Puma Energy

Tulimkamata Malima eneo la mjini linaloitwa pasians na baadae aliachiwa baada ya kuhojiwa na kuonekana hakuna ushahidi wa kumpeleka mahakamani

Baada ya hapo upelelezi uliendelea na tarehe 22/11 aliketwa mtuhumiwa wa nne Freeman Mbowe ili niweze kumuhoji

Baada ya mtuhumiwa kuletwa mbele yangu na kujitambulisha nilimuonya kuhusiana na tuhuma za kula njama za kutenda ugaidi na baada ya kumuonya alikubali kuandika maelezo yake mbele ya Wakili wake alimtambulisha Fred Khiwelo.

Wakili Kibatala: Haya yote anayoeleza shahidi yako kwenye rekodi sioni kama yana tija

Shahidi: Baada ya kumuhoji Mbowe alisema hawezi kutoa maelezo hadi pale atakapofika mahakamani.

Jina la Alfani Bwire nililiandika kutokana na matamshi yake mwenyewe

Mheshimiwa Jaji ni hayo tu.

Wakili Kibatala:  Kutokana na yale mazoea yetu tuliyojiwekea kupumzika saa saba ningeshauri tupumzike dakika 45 ili tukirudi tuweze kuendelea

Wakili Kidando: Mheshimiwa hatuna pingamizi

Jaji. Tunabreak kwa dakika 45 tutarudi hapa saa saba na nusu.

…………………………………………………..


Mahakama imerejea kwaajili ya upande wa utetezi kumuhoji Shahidi.

Wakili Nashon Nkungu: Unasema ulihusika kuwakamata mshtakiwa wa pili na watatu

Shahidi: Ni sahihi

Wakili: Baada ya kuwakamata mlienda nao central Polisi

Shahid. Ndio

Wakili. Mlikuwa na afande Mahita

Shahdi: Ndio

Wakili: Mlifika kituoni

Shahid: Ndio

Wakili: Mwambie Jaji kama ni muhimu kumuandikisha mtuhumiwa kwenye detention register

Shahidi: Ndio

Wakili: Kwahiyo unaweza kumfikisha mtuhumiwa kituoni na usimwandikishe

Shahidi: Mtuhumiwa anaandikishwa pale anapofikishwa kituoni

Wakili: Unafahamu kwamba ni kinyume na PGO inapinga askari kutegemea kumbukumbu zake kwenye kesi za jinai

Shahidi: Hiyo ni nyongeza

Wakili: Muda nni vitu vya makadirio au ni muda sahihi


Shahidi: Ni Muda sahihi


Wakili: Mida mliyokuwa mna andika ni sahihi na sio makadirio

Shahdi: Ni Muda sahihi

Wakili: Ulisema mlifika Rau madukani saa saba mlifika na dakika ngapi?

Shahidi. Nachojua tulifika saa saba sio kila nachofanya ntaangalia dakika.

Wakili: Baada ya kufika pale mahita aliambiwa akaangalie kama mtuhumiwa wa pili na Watatu wako pale

Shahidi: Ni sahihi

Wakili: Ilikuwa saa ngapi

Shahii: Sio kila unachofanya unakadiria muda

Wakili: Nikisema alirudi baada ya nusu saa

Shahidi: We ndio utakuwa umesema hivyo

Wakili: Mazoezi yote sita yalifanyaika kwa muda gani

Shahidi: Ndani ya saa moja

Wakili: Baada ya kufanyika mambo yote mlienda kuwapekuea

Shahid: Ndio

Wakili: Hebu mwambie Jaji hii immrandikwajr

Shahidi: P12

Wakili: Na hii nyingine unaweza kutambua

Shahidi: Imeandikwa P11

Wakili. Kwenye vielelezo hivi angalia upekuzi ulifanyika muda gani

Shahidi: Saa saba mchana.

Wakili: Upekuzi ulifanyika kabla hamjafika?

Shahidi: Ulifanyika saa saba mchana

Wakili. Ni sahihi zaidi ya mara moja mlienda na watuhumiwa Moshi central

Shahidi: Kweli

Wakili: Ni sahihi kwamba mlitembea na watuhumiwa na kuwarudisha polisi, huoni kama mngepata nguvu kama mngetoa detention register

Sahahid: Muhimu ni ushahidi nilioutoa hapa

Wakili: Unajua umuhimu wa detention register

Sahahid: Ndio

Wakili: Bila kuwepo kwa nyaraka hizi mtu anaweza kuwa na uhakika watuhumiwa walifikishwa polisi

Shahidi: Sio lazima mtu aliyefikisha ndio anaweza kusema

Wakili: Kwahiyo hata muda wa uwakika kuletwa Dar haupo

Shahidi: Upo

Wakili: Kwahiyo hata nyaraka hiyo hujaileta hapa mahakamani

Shahidi: Sijaileta

Wakili: Mkiwa moshi watauahumiwa walilala wapa

Shahidi: Sijui kama walilala kwa kuwa kituo cha polisi

Wakili: Kama kweli mlisafiri kitu kingine cha kuonyesha ni polisi logbook

Shahidi: Polisi logbook hainihusu mimi sio dereva

Wakili: Mlisafiri na gari binafsi au ya Polisi

Shahidi: Ya Polisi

Wakili: Kila safari unajua lazima iwe autorised

Shahidi: Nafahamu

Wakili: Unafahamu unapoanza kusafiri station ofiser anatakiwa kurekodi muda na namba ya gari

Shahidi: Inategemea

Wakili: Unafahamu gari ya Polisi inapotoka nje ya mkoa unahitaji ruhusa ya IGP

Shahidi: Sio kweli

Wakili: Unafahamu gari inapopata hitilafu inatakaiwa kuripotiwa kituo cha karibu

Shahidi: Sio kweli

Wakili: Unafahamu fomu ya Polisi EMI

Shahidi: Sifahamu

Wakili: Unajua gari ya Polisi inataikiwa kuwa na logbook

Shahidi: Nafahamu

Wakili: Ni sahihi hujatoa logbook hapa mahakamani

Shahaidi: Sijato

Wakili: Na kwenye ushahid wako hujataja namba za gari

Shahidi: Sijataja

Wakili: Tarehe 9 wewe na Mahita mliwapeleka watauahumiwa Mbweni

Shahidi: Sio kweli

Wakili: Unakumbuka nmba za gari mliotumia

Shahidi: Sikumbuki

Wakili: Ili kuonyesha mlienda Mbweni una logbook

Shahidi: Mimi sio dereva

Wakili: Kuna kauli mbili za mashahidi wawili ni sahihi wewe na Mahita mlikuwa kwenye gari moja

Shahidi: Ni sahihi

Wakili: Mlikuwa mnawauliza maswali mbalimbali.

Shahidi: Vitu gani hebu fafanua

Wakili: Mahita alihoji alipo mtuhumiwa Lijenje

Shahidi: Hilo liliulizwa

Waikili: We na Mahita nani muongo

Shahidi: Hakuna muongo

Wakili: Unajua watuhumiwa wanakataa hamkuzunguka kutafuta mtumiwa mwingine

Shahidi: Kwenye ushahidi wangu nimeeleza

Wakili: Mlienda hadi Aish hotel

Shahidi: Tulienda

Wakili: Mlikuwa na hati ya upekuzi

Shahidi: Hatukwenda kupekua tulienda kutafuta mtuhumiwa

Wakili: Uliiingia kwenye hiyo hoteli

Shahidi: Alienda Kiongozi wetu

Wakili: Kama mlikuwa mnamtafuta mtuhumiwa mlienda tu na kuondoka

Shahidi: Hiyo ni kazi inayohitaji utaalamu sio kama unavyotaka wewe

Wakili: Ulisema sababu za kutokuandika maelezo ni kwakuwa mlikuwa a mnamtafuta Lijenje

Shahidi: Pamoja na shauri lilipokuwa limefunguliwa Dar es salaam

Wakili: Wakati huo mlikuwa mnamfahamu mtuhumiwa wa nne Freeman Mbowe ni mtuhumiwa

Shahidi: Tulikuwa tunafahamuu

Wakili: Wengine waliweza kuandika bila Mbowe kukamatwa

Shahidi: Ni sahihi

Wakili: Ni sahihi Mbowe ulimuhoji saa sita usiku

Shahidi: Ndio

Wakili: PGO inaeleza kila hatu zichukuliwe kwenye ushahidi utakaohusu finger print

Shahidi: Ni sahihi

Wakili: Ni sahihi hapa mahakamani hujaleta ushahidi unaohusu finger print

Shahidi: Ndio haikuwa na sababu

Wakili: Unafahamu madawa ya kulevya yakikamatwa yanatakiwa kumkabidhiwa kituo cha karibu

Shahidi: Inategemea na mazingira

Wakili: Unafahamu mtuhumiwa akikiri anatakiwa kupelekwa kwa mlinzi wa amani

Shahidi: Inategemea na mtuhumiwa mwenyewe

Wakili: Unafahamu mtu huyo wa tatu anaongeza nguvu mahakamani

Shahidi: Nafahamu

Wakili: Kwahiyo hukuona umuhimu wa mlinzi wa amani

Shahidi: Kama nilivyosema inategemea na uhitaji wa mtuhumiwa

Wakili: Mahita si unamfahamu

Shahidi. Nafahamu

Wakili: Ulimtaja ni mmoja mlieenda naye nyumbani kwa Bwire

Shahidi: Ndio

Wakili: Kwenye ushahidi wako mlimkamata Bwire na simu mbili

Shahidi: Ni sahihi

Wakili: mmezitoa hapa mahakamani

Shahidi: Hapana

Wakili: Mnazihusisha na tuhuma hizi za ugaidi

Shahidi: Bado ziko kwenye utaratibu

Wakili Nkungu amemaliza sasa ni zamu ya Wakili John Mallya.

Wakili Mallya: Unajua mamlaka inayotoa leseni ya kufanya biashara ya mafuta

Shahidi: Sifahamu

Wakili. Inaitwa EWURA

Wakili: Hata kama hujui EWURA wanatoa leseni lakini wale wanaofanya biasahara wanaopata wapi leseni

Shahidi. Sifahamu

Wakili: Umekuja na barua kutoka EWURA angalau Jaji ajue Mwanza Pasians pana kutuo cha Puma Energy

Shahidi: Mimi sijasema kama pana kutuo cha mafuta

Wakili: Mwambie Jaji kama wewe unatoa leseni

Shahidi: Sitoi leseni

Wakili: Twende kwenye siko hapo ulipozungumzia pana soko

Shahidi: Lipo

Wakili: Unasjili masoko

Shahidi: Hapana

Wakili: Umewahi kufanya kazi ofisi ya DIC kabla ya kwenda Arusha

Shahidi: Ndio

Wakili: Ulikuwa kitengo gani

Shahidi: Kitengo cha upelelezi

Wakili: Umewahi kushiriki operesheni mbalimbali

Shahidi: Ndio lakini siwezi kuzitaja

Wakili: Ushiriki wako kwenye kesi ya Tito Magoti

Shahidi: Siwezi kulizuungumzia hapa

Wakili: Unajua Freeman Mbowe ni kiongoz wa upinzani

Shahidi: Ndio

Wakili: Amekuwa akipingana na Sera za Serikali

Shahidi: Siwez kulizuungumzia

Wakili: Umesema wewe ni msukuma unajua na Boazi naye ni Msukuma

Shahidi: Sifahamu

Wakili: Na kwenye kesi ya Kabendera ulihusiakaje

Shahidi: Sifahamu

Wakili: Umesema mnashirikiana na serikali za mita unajua mtuhumiwa wa nne aliwahi kuambiwa anauza madawa ya kulevya na kina Makonda

Shahidi: Sifahamu

Wakili: Umewahi kusikia kuhusu kupotea kwa Beni saa nane

Shahidi: Nilisikia kwenye vyombo vya habari

Wakili: Mlimpeleka wapi Beni

Shahidi: Sifahamu

Wakili: Mbowe alivyokamtwa aliletwa kwako

Shahidi: Ndio

Wakili: Vitu vya Mbowe zikiwemo simu ziko wapi

Shahidi: Sifahamu….

Wakili: Watuhumiwa wanadaiwa kufanya vikao vya ugaidi Dar hebu nionyeshe kwenye maelezo yako wapi wamekiri

Shahidi: Anasoma maelezo

Wakili: Kujadiliana kuhusu malipo ni vikao vya ugaidi

Shahidi: Ndio

Wakili: Unajua sheria inakataza mtu kuwa na mlinzi binafsi

Shahidi: Ndio

Wakili: Ukiwa kwenye ofisi ya DCI 2017 Kiongozi mwenzake Tundu Lissu alivamiwa na risasi

Shahidi: Nafahamu

Wakili: Na unafahamu watu wanaoweza kutumia silaha kama hizo ni watu wenye mafanzo

Shahidi: Hata wahalifu wanaweza

Wakili: Sasa mtu kama Mbowe hutaki ajilinde

Shahidi: Ni kazi ya Polisi

Wakili: Wakati Lissu anavamiwa polisi walikuwa likizo?

Shahidi: Lilikuwepo

Wakili: Sasa kuna ubaya gani

Mbowe kujilinda

Shahidi: Hakuna ubaya

Wakili: Bastola uliyosema ulikama kwa Adamoo inamilikiwa na Kingai na wewe ndio uliweka

Shahidi: Sio kweli

Wakili: Bastola hiyo inamilikiwa na Kingai na aliinunua 2014 pale Moshi ndio maana Msajili hakuleta rekodi zake hapa

Shahidi: Siwezi kuliongelea

Wakili: Ulishawahi kutoa maelezo yoyote kuhusiana na jina Adamoo

Shahidi: Sijaelezea

Wakili: Mheshimiwa ni hayo tu





Wakili Dickson Matata anaanza kumuhoji Shahidi.

Wakili Matata: Ling'wenya alienda kwa Mbowe kufanya nini?

Shahidi: Alisema alipigiwa simu na Denisi Urio kwaajili ya VIP Protection

Wakili: Ni kosa au sio kosa kufanya VIP Protection

Shahidi: Sio vibaya kama itafanyika hivyo

Wakili: Na huyu mtu alitumiwa nauli

Shahidi: Ndio

Wakili: Ni kosa mtu kutumia fedha ya nauli na kula njiani

Shahidi: Sio kosa kama itakuwa imetumika hivyo

Wakili: Naomba nikuulize kuna sehemu yoyote imetajaa vituo vya mafuta au sheli

Shahidi: Hivijatajwa

Wakili: Naomba nionyeshe ni wapi pameandikwa wataweka sehemu gani magogo

Shahidi: Hakuna

Wakili: Ni sehemu gani specific wamesema watafanya maandaman

Shahidi: Hakuna

Wakili: Ni kosa kufanya maandamano kwa mujibu wa sheria

Shahidi: Inategemea yanafanyikaje

Wakili Matata: Ni kifungu gani kinasema mtuhumiwa kupelekwa kwa mlinzi wa amani hadi atake

Shahidi. Sikumbuki ila ni kwa uelewa wangu

Mheshimiwa ni hayo tu

Sasa ni zamu ya Wakili Peter Kibatala.

Wakili Kibatala: Kupitia kesi hii unajua Watanzania wanapima utendaji kazi wa Jeshi la Polisi

Shahidi: Mimi natimiza majukumu yangu

Wakili: Unafahamu unatakiwa kuwa na adabu mbele ya mahakama

Wakili: Mheshimiwa Jaji tarehe 14/12 uje na udhibitisho tarehe 15 Desemba ulifanya au hukufanya

Shahidi: Sikufanya

Wakili: Sasa unataka tukuelewe kuwa una adabu mbele ya washtakiwa na mahakama

Shahidi: Ni nayo adabu

Wakili: Ulinyosha mkono ukasema kuna swali hujaulizwa

Shahidi: Sikunyoshaa

Wakili: Kwahiyo tuseseme umeizoea sana mahakama

Shahidi: Hapana

Wakili: Mwaka 2020 ulikuwa na cheo cha ASP

Shahaidi: Ndio

Wakili: Ni lini ulipandishwa

Shahidi: Mwaka jana mwezi sita

Wakili: Kupandisha cheo ilikuwa tayari umeshiri kwenye masuala ya upelelezi kwenye kesi hii

Shahidi: Ndio

Wakili: Kipindi kile alikuwa na cheo gani

Shahidi: ASP

Wakili: Na alikuwa nani

Shahidi: Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha

Wakili: Na sasa hivi

Shahidi: RPC

Wakili: Mahita sasa hivi ni nani

Shahidi: Inspekta

Wakili:  Alipanda au ameshuka

Shahidi: Amepanda

Wakili: Na Goodluck

Shahidi: Yuko chuo anasoma

Wakili: Kukamatwa kwa Bwire dereva wa daladala unamfahamu

Shahidi: Siwafahamu

Wakili: Hukuchukua taarifa zozote

Shahidi: Hapana

Wakili: Sasa huoni utatupa ugumu kujitetea

Shahidi: Kwenye ushahidi wangu nimeeleza

Wakili: Tutakuaminije wakati uliambiwa ulete vyeti hujaleta.

Shahidi: Mshtakiwa alikamatwa ndio maana yuko chini ya ulinzi

Wakili: Hata details za trafiki aliyeelekeza daladala

Shahidi: Haikuwa na umuhimu



Wakili: Ni sahihi ulipohojiwa ulimzungumzia simu za Bwire wakati zinachukuliwa ulikuwepo

Shahidi: Nilishuhudia

Wakili: Wakati mnazichukua kulikuwa na shahidi huru yoyote

Shahidi: Hapana

Wakili: PGO inasemaje kuhusu shahidi huru yoyote

Shahidi: Kuwepo na shahidi huru

Wakili: We ndio una panga shahid gani anakuja

Shahid: Mimi sikuhusika na hizo simu

Wakili: Kwa ufahamu wako washtakiwa walioachiwa walikaa ndani muda gani

Shahidi: Muda mrefu karibia mwaka mmoja

Wakili: Kwanini mliwaachia

Shahidi: Upelelezi ulikamilika

Wakili: Polisi wamejipangaje kuwa fidia

Shahidi: Siwezi kulizungumzia

Wakili: Kuna mmoja hadi leo amepata tatizo la kiakili

Shahidi. Sifahamu

Wakili: Unajua hawa vijana walitumikia hii nchi kwa jasho na damu

Shahidi: Walikuwa ni wahalifu

Wakili: Kwanini mliwaachia

Shahidi: Ushahidi haukutosheleza

Wakili: Kwanini mahakama isione wewe una maslahi

Shahidi: Sina maslahi

Wakili: Ulisema matendo haya ya kigaidi yalikuwa yafanyike nchi nzima

Sahahid: Ni sahihi

Wakili: Kwahiyo wahanga wangekuwa pamoja na raia wa kigeni

Sahahid: Inawezekana

Wakili: Mlitoa taarifa kwa Ubalozi wowote

Shahidi: Hapana

Wakili: Unajua mapambano ya ugaidi ni ya Kimataifa na kuna mkataba mbalimbali tumesaini

Shahidi: Ndio

Wakili: Mwambie Jaji kama ulimzungumzia jitihada zozote mlizofanya na Interpol

Shahidi: Suala hilo sikulizungumzi

Wakili. Ulimwambia Jaji Soko la Kilombero liko moja tu

Shahidi: Sikumwambia

Wakili: Sheli ni nini

Shahidi: Watatu wamezoea kutumia jina hilo

Wakili: Wakati wanatoka Morogoro kwenda Moshi walikuwa wanafahamu kuwa wanaenda kufanaya vitendo vya kigaidi

Shahidi: Walikuwa wa nafahamu

Wakili: Kati ya Mbowe na Urio nani alikuwa anawafahamu

Shahidi: Aliyekuwa anafadhili

Wakili: Mbowe na Urio nani alikuwa Morogoro

Shahidi: Urio

Wakili: Nani aliyewatongoza

Shahidi. Urio

Wakili. Urio ni mtoto mdogo

Shahidi: Mtu mzima

Wakili: Urio yuko hapa kizimbani

Shahidi: Hayupo

Wakili: Mheshimiwa Jaji kama wenzangu watakubali naomba niahirishe tuendelee tena kesho kwa kuwa nina maswali mengi.

Wakili Kidando: Hatuna pingamizi na tulishakubaliana naomba tuahirishe shauri hili hadi kesho.

Jaji: Kufuatia maombi yaliyoletwa na upande wa utetezi na kuridhwa na upande wa mashtaka naahirisha shauri hili hadi kesho saa tatu asubuhi ambapo upande wa utetezi wataendelea kumuhoji shahidi, shahidi unaonywa kuwa kufika kwaajili ya kuendelea kutoa ushahidi na washtakiwa mtaendelea kuwa chini ya uangalizi wa magereza.