Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kigamboni waanza operesheni kudhibiti panya road

Muktasari:

  • Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Fatma Nyangasa amekutana na wenyeviti wa Serikali za mitaa wa wilaya hiyo, huku akiwaonya vijana waliopanga kufanya uhalifu akisema polisi imeanza operesheni ya kukabiliana na vitendo hivyo.


Dar es Salaam. Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni, Fatma Nyangasa amekutana na wenyeviti wa Serikali za mitaa wa wilaya hiyo, huku akiwaonya vijana waliopanga kufanya uhalifu akisema polisi imeanza operesheni ya kukabiliana na vitendo hivyo.

Mkutano wa Nyangasa na wenyeviti hao pamoja na wajumbe kamati ya ulinzi na usalama umefanyika leo Alhamisi Septemba 15, 2022 katika ofisi ya mkuu wa huyo. Nyangasa amewaelekeza wenyeviti hao kuhakikisha ulinzi shirikishi unafanyika kikamilifu na kutoa taarifa ya hali ya usalama katika maeneo yao.

"Kuanzia leo tumeanza operesheni maalumu katika maeneo na mitaa yote ya Kigamboni. Nyie (wenyeviti) ni viongozi kwenye mitaa kwa hiyo mtashiriki hili kikamilifu.

" Lengo kuhakikisha hakuna mtu mwenye nia au mipango ya kufanya  uhalifu kwa  Wanakigamboni. Jukumu letu kuwalinda wananchi wa Kigamboni, sote tuwajibike, polisi wataingia mitaani na viongozi tushirikiane kwa kutoa taarifa sahihi," amesema Nyangasa 

Mkuu wa Polisi wilaya ya Kigamboni, ( OCD) Thobias Walelo amesema timu yake ipo tayari kuhakikisha  ulinzi na usalama unaendelea kuimarika Kigamboni, huku akiwataka wananchi kutoa ushirikiano katika upatikanaji taarifa za watu au kikundu kinachojihusisha  vitendo vya uhalifu.