Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Maimu, wenzake wasomewa mashtaka 100

Muktasari:

  • Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dickson Maimu na wenzake watano wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa mashtaka mapya 100, yakiwamo ya kufanya udanganyifu

Dar es Salam. Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Dickson Maimu na wenzake watano, wamepandishwa  katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam kijibu mashtaka mapya 100, yakiwamo ya kufanya udanganyifu.

Akisoma hati ya mashtaka leo Jumanne Januari 29, 2019, Wakili wa Serikali Simon Wankyo akisaidia na Leoanard Swai mbele ya hakimu  Salum Ally, amedai washtakiwa wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 7 /2019.

Washtakiwa wanadaiwa kughushi na kufanya udanganyifu katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), hivyo kuisababishia Serikali hasara ya Sh1.1 bilioni.

Endelea  kufuatilia Mwananchi kujua undani wa mashtaka hayo katika kesi inayoendelea mahakamani hapo