Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Rais Samia ateua bosi jeshi la polisi

Kamishna wa Polisi, Suzan Kaganda

Muktasari:

Suzan Kaganda anachukua nafasi ya Kamishna wa Polisi (CP), Benedict Wakulyamba ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amempandisha cheo Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), Suzan Kaganda kuwa Kamishna wa Polisi.

 Taarifa iliyotolewa leo Jumatatu Oktoba 24, 2022 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Zuhura Yunus imeeleza Amri Jeshi Mkuu huyo wa vikosi vya ulinzi na usalama pia, amemteua Kamishna Kaganda kuwa Kamishna wa Utawala na Raslimali watu wa Jeshi la Polisi.

“Vile vile, Rais Sarnia amemteua Kamishna Kaganda kuwa Kamishna wa Utawala na Raslimali watu wa Jeshi la Polisi,” imesema taarifa hiyo.

Kamishna Kaganda anachukua nafasi ya Kamishna wa Polisi (CP), Benedict Wakulyamba ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Taarifa hiyo imesema kuwa uteuzi huu unaanza mara moja.