Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Serikali yaeleza faida za urasimishaji ardhi

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula

Muktasari:

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula amesema hayo alipojibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Salma Mwassa aliyetaka kujua umuhimu wa kurasimisha ardhi maeneo ambayo hayajapimwa.

Dodoma. Mipango hiyo, kwa mujibu wa Serikali inapaswa kwenda sambamba na uimarishaji wa usimamizi na udhibiti wa uendelezaji wa mandhari ya nchi.

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula amesema hayo alipojibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Salma Mwassa aliyetaka kujua umuhimu wa kurasimisha ardhi maeneo ambayo hayajapimwa.

 Mabula amesema urasimishaji huo maana yake ni kutambua miliki za wananchi kwenye maeneo yaliyoendelezwa bila kupimwa kisheria.

“Urasimishaji ni kazi shirikishi inayowezesha wananchi kukubaliana mipaka ya viwanja, kufungua njia na kutoa maeneo ya huduma za jamii kama vile shule, vituo vidogo vya polisi, makaburi, zahanati na maeneo ya wazi,” amesema.