Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Tanapa yaja na mkakati kudhibiti uvamizi wa tembo

Tanapa yaja na mkakati kuthibi uvamizi wa tembo

Muktasari:

  • Tanapa yajipanga kuondoa tatizo la tembo kuua watu na kuharibu mazao shambani.

Katavi. Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini  Shirika la hifadhi za taifa Tanzania (Tanapa) Jenerali Mstaafu George Waitara amesema shirika hilo linajipanga  kuliondosha tatizo la tembo kuua watu na kuharibu mazao shambani .

Waitara amebainisha hayo alipokuwa  akifunga mafunzo ya ajira mpya “Recruit Course” kwa wahitimu 57 Tanapa yaliyofanyika kituo cha Mlele mkaoni Katavi.

 Akiwahutubia wahitimu hao amesema maliasili zinahujumiwa na majangili japo kwa sasa  tatizo hilo limedhibitiwa kwa kiasi kikubwa hasa kuzuia ujangili wa tembo.

“Sasa hivi hata huku  mnasikia kulalamikiwa kila wakati tembo wapo vijijini, wengine huwa wanasema tembo wameongezeka inashangaza katika kipindi kifupi tembo wanaweza kuzaliana kiasi hicho haiwezekani?,amesema Waitara

Amesema awali tembo walikuwa wametawanyika na kwamba  wamerudi kwasababu wana amani na waliosababisha amani hiyo ni jitihada za askari wa Tanapa.

“Hizi changamoto za kuua watu kula mazao tutajua namna ya kuziondosha,tembo ni mnyama mwenye akili sana anapita maeneo aliyopita miaka hamsini iliyopita, binadamu tunaongezeka hatujui tupo kwenye maeneo yao, amerudi anafuata mlemle,rai yangu mnakokwenda endeleeni kuelimisha ,”amesema.

Awali akisoma taarifa ya mafunzo ya askari  wa ajira mpya  Mhifadhi Mwandamizi Makao makuu Emmanuel Kaaya amesema wahitimu hao wamefanikisha kukamata majangili 19 na gobore tatu katika hifadhi ya Katavi.

“Pia walikamata ng’ombe 440,wachungaji 18,mbwa wawili  waliuua,unga wa gobore gm 500 na  risasi 42,,shoka 8,baiskeli 7, misumeno ya mbao 2,panga 7,visu 4, nyama pori gm 100 na ya nguruwe kilo 70,’amesema Kaaya .

Ameongeza kuwa sh 46 milioni zimepatikana baada ya watuhumiwa kukamatwa na kupigwa faini akidai kuwa wahitimu waliofanyia mafunzo yao ya vitendo katika hifadhi ya taifa Serengeti wamefanikiwa kutegua nyaya za mitego 239 na kukamata majangili 14.

Baadhi ya wahitimu wa mafunzo hayo Anderson Anton na Fartuma Hamis waliotunukiwa vyeti kwakufanya vizuri  darasani wameeleza mbinu walizozitumia ni kusikiliza kwa umakini walivyokuwa wakifundishwa.

“Tuwashukru wakufunzi wetu wametufundisha vizuri na siyo kwamba tumekuwa bora wawili tu hapana wote tumefanya vizuri lakini ilitakiwa wapatikane wawili,”wamesema.