Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Wahitimu NIT washauriwa kutumia ubunifu kutengeneza ajira

Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC,) Abdi Mkeyenge

Muktasari:

  • Wahitimu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) wameshauriwa kutumia ubunifu na maarifa waliyoyapata kutengeneza ajira sio kutegemea kuajiriwa pekee.

Dar es Salaam. Wahitimu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) wameshauriwa kutumia ubunifu na maarifa waliyoyapata kutengeneza ajira sio kutegemea kuajiriwa pekee.

Wito huo umetolewa jijini Dar es Salaam leo Jumamosi Desemba 4, 2021 na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Abdi Mkeyenge wakati wa maadhimisho ya Kongamano la nane la wahitimu wa chuo hicho hicho.

Katika kongamano hilo ilibainisha malengo yake ya ushindani katika kuwandaa wanafunzi wenye ujuzi na ubunifu watakaoweza kutengeneza ajira kupitia fursa ambazo Serikali imezitangaza ikiwemo uchumi wa Buluu, ujenzi wa bwawa la kufua umeme la Mwalimu Nyerere na ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Tanga Tanzania.

Akizungumza katika kongamano hilo, Mkeyenge amesema wanapaswa kutumia  ubunifu na maarifa wanayofundishwa chuoni hapo kwa manufaa ya jamii nzima.

“Tuache kabisa dhana ya kuajiriwa bali tufikilie zaidi kujiajiri, najua ujuzi, maarifa na tafiti mlizozipata hapa chuoni ni nyenzo kubwa kwetu katika kutengeneza jira, zinduka sasa na chukua hatua ya kujiajiri pale unapoona fursa ya kufanya hivyo,” amesema

Awali akizungumza katika Kongamano hilo Mkuu wa Chuo cha NIT, Profesa Zacharia Mganilwa amesema kongamano hilo limelenga kuwakutanisha walimu, wanafunzi na wahitimu kwa kuwaonesha dira baada ya kuhitimu na namna ya kutumia maarifa waliyoyapata kwa vitendo.