Luteni Urio: Sikuona umuhimu kurekodi mazungumzo yangu na Mbowe

New Content Item (1)
New Content Item (1)

Muktasari:

  • Shahidi wa 12 Luteni Denis Urio amesema hakuona umuhimu kurekodi mazungumzo yake na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe baada ya kuulizwa na mmoja wa mawakili wa utetezi kwa nini hakufanya hivyo

Dar es Salaam. Shahidi wa 12 Luteni Denis Urio amesema hakuona umuhimu kurekodi mazungumzo yake na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe baada ya kuulizwa na mmoja wa mawakili wa utetezi kwa nini hakufanya hivyo

Shahidi huyo wa Jamhuri katika kesi ya ugaidi inayomkabili Mbowe na wenzake watatu amesema hayo leo Alhamisi Januari 27, 2022 alipokuwa akiulizwa maswali na wakili wa utetezi Nashon Nkungu.

Soma maswali ya mawakili wa utetezi na majibu ya shahidi

Mahakama imerejea kwa ajili ya Jaji Joachim Tiganga kutoa uwamuzi baada ya Wakili wa utetezi Nashon Nkungu kuiomba Mahakama hiyo kutoa maelekezo kwa Shahidi wa 12 Luteni Denis Urio kujibu baadhi ya maswali ambayo alisema hawezi kuyajibu kutokana na kiapo chake cha kazi.

Baada ya Wakili Nkungu kuiomba mahakama kutoa maelekezo kwa shahidi kujibu maswali Jambo hilo liliibua mvutano wa kisheria uliosababisha Jaji Tiganga kuahirisha mahakama kwa muda kwa ajili ya kwenda kupitia vifungu mbalimbali vya sheria.

Tayari Mawakili wa pande zote wamejitambulisha, kutokana na kolamu zao kutobaadilika pande zote ziko tayari kwa uwamuzi.

Jaji ameanza kusoma uwamuzi kwa kupitia hoja zilizowasilishwa na pande zote

Jaji: Mahakama imekubaliana na maombi ya upande wa utetezi na kuelekeza Wakili anapomuuliza swali shahidi kulenga mambo yanayomuhusu Shahidi binafsi.

Wakili Nashon: Shahidi unakumbuka swali nililokuuliza?

Shahidi: Sikumbuki

Wakili Nashon: Nimekuuliza Levo yako ya ukomandoo

Shahidi: Mheshimiwa Jaji naomba nimpigie muajiri wangu simu kwanza

Jaji: Utakapoulizwa sema mahakama imenitaka nijibu

Shahidi: Nina Advance diploma ya parachuti

Wakili Nashon: Unaweza kukumbuka askari waliokuwepo kwenye mishe I Sudani 2011

Shahidi: Siwezi kukumbuka

Wakili Nashon: Na idadi ya askari waliokuwepo

Shahidi: Siwezi kukumbuka

Wakili Nashon: Na kwa Mwaka 2019

Shahidi: Siwezi kukumbuka

Wakili Nashon: Wakati Halfani Bwire alifukuzwa hukuwepo Tanzania

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Nawakati Ling'wenya anafukuzwa hukuwepo

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Nitakuwa sahihi ulikuwa na nia ovu kuzungumzia matukio ya hawa washtakiwa wakati hukuwepo

Shahidi: Sio sahihi

Wakili Nashon: Ni sahihi hufahamu kwa undani suala lililowafanya kufukuzwa kazi

Shahidi: Utovu wa nidhamu

Wakili Nashon: Utovu wa nidhamu sio kosa ila ndani yakee ndio kosa

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Kwahiyo hufahamu Halfan Bwire alifukuzwa kwa kosa gani

Shahidi: Sio jukumu langu

Wakili Nashon: Hujataja hatua wa makosa yaliyosababisha wao kufukuzwa

Shahidi: Sijata

Wakili Nashon: Hujataja aliyewafukuza

Shahidi: Sifahamu.

Wakili Nashon: Huwezi kufahamu siku na tarehe waliofukuzwa

Shahidi: Sifahamu

Wakili Nashon: Ni kweli hukutaja jina la huyo admin Ofisa aliyeekupa hizo taarifa.

Shahidi: Sikutaja

Wakili Nashon: Ni sahihi hukusema aliyekupa taarifa ni zaidi ya Admin Ofisa mmoja

Shahidi: Nilienda ofisini na kupitia mafaili na sio mtu aliyenipa taarifa.

Wakili Nashon: Huwezi kuiambia mahakama hawa walifukuzwa kazi kama hujataja aliyewafukuza

Shahidi: Waliofukuzwa na muajiri wao

Wakili Nashon: Unakumbuka siku mliyokutana na Freeman Mbowe Mikocheni

Shahidi: Ndio

Wakili Nashon: Wakati anakueleza mipango yake ulikuwa na akili timamu?

Shahidi: Ndio

Wakili Nashon: Muda huo ulikuwa hujawasilia na chombo chochote cha ulinzi

Shahidi: Ilikuwa bado

Wakili Nashon: Ni kisema kile kikao na wewe ulikaa kikao cha ugaidi utakubali

Shahidi: Sio sahihi

Wakili Nashon: Ni sahihi baada ya kile kikao ulikubali kwenda kumtafutia watu kutokana na ulikuwa na uchu wa  madaraka

Shahidi: Sio sahihi sikuomba cheo

Wakili Nashon: Ni sahihi jeshi kuna kitu kinaitwa chini of information

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Inahusisha kutembea kwa taarifa

Shahidi: Hatutegemei taarifa

Wakili Nashon: Mgulani ni kambi ya jeshi?

Shahidi: Ni rest za jeshi

Wakili Nashon: Unapopata taarifa ni lazima upeleke kwa information officer

Shahidi: Sio lazima

Wakili Nashon: Wewe askari unapopata taarifa hutakiwi kupeleka kwa intelligence offers

Shahidi: Naomba kutoa maelezo unapopata taarifa kama hizi unatoa taarifa za haraka

Wakili Nashon: Jambo nyeti kama hili unakumbuka tarehe

Shahidi: Tarehe sikumbuki

Wakili Nashon: Ni muhimu unapoenda kwenye Ofisi za umma kujiandikisha

Shahidi: Sikujuandikisha nlitoa kitambulisho wakanitambua

Wakili Nashon: Ulisema Mbowe alisema anataka kuchukua dola

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Bila hata uchaguzi

Wakili Nashon: Alisema kwa kukata miti

Shahidi: Ili kuleta taharuki

Wakili Nashon: Mbowe angetaka kuchukua nchi ni kuchukua wanajeshi waliofukuzwa au kuchukua walioko kazini

Wakili Chavula: Naomba hilo lisiingie kwa kuwa anatafuta maoni ya shahidi.

Wakili Nashon: Baada ya makubaliano yale ulimtafuta Bwire na kumueleza kuwa Mbowe anatafuta walinzi

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Na moyoni ukiwa unafahamu Mbowe anaenda kufanya ugaidi ukaniambia Bwire kuwa Mbowe anatafu mlinzi

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Na ukafanya hivyo kwa mshtakiwa wa kwanza na wa pili

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Kwa hiyo uliwadanganya washtakiwa

Shahidi. Sukudanganya niliwaambia

Wakili Nashon:  Ulisema ulikutana na mshtakiwa wa kwanza wa pili na watatu Morogoro

Shahidi: Ni sahihi.

Wakili Nashon: Hebu isaidie mahakama kama unafahamu muda mwingine wowote mshtakiwa wa kwanza hadi wa nne walikutana Morogoro kula njama hizo  

Shahidi: Sifahamu

Wakili Nashon: Vipi kuhusu na Moshi Aishi hoteli

Shahidi: Sifahamu

Wakili Nashon: Na Arusha

Shahidi: Sifahamu

Wakili Nashon: 2012 ulikuwa na renki gani

Shahidi: Koplo.

Wakili Nashon: Na ulivyokutana na Mbowe ulimwambia huna renk yoyote

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Jibu ulilompa lilikuwa ni sahihi

Shahidi: Kwangu mimi lilikuwa sahihi

Wakili Nashon: Ulisema hufungamani na chama chochote isipokuwa Kiongozi alioko madarakani

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Kwa hiyo ni ushahidi wako hukusema ni Kiongozi gani Rais au Mkuu wa Wilaya

Shahidi: Nilisema naheshimu mamlaka zilizoko madarakani

Wakili Nashon: Ulikuwa ukiwasiliana na Mbowe kwa njia ya simu

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Ulipoenda kwa DCI ulipewa mpelelezi gani

Shahidi: Kingai

Wakili Nashon: Wakati unawapa taarifa Kingai na DCI uliwaambia Mawasiliano yenu makubwa ni kwa njia ya simu

Shahidi: Niliwaambia

Wakili Nashon: Na wewe umewasilisha simu zako nne hapa mahakamani

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Hapakuwa na umuhimu wa kurekodi wakati wote mnaongea

Shahidi: Sikuona umuhimu

Wakili Nashon: Unaweza kueleza meseji hata moja kati ya ulizosoma yenye muelekeo wa ugaidi

Shahidi: Mtu mbili au tatu wanahitajika haraka ni meseji ya kwanza.

Wakili Nashon: Naomba kupatiwa kielezo namba 23. Shahidi naomba nitafutie meseji yenye kupanga ugaidi msomee Jaji.

Shahidi: Kaka zile mtu mbili au tatu zinahitajika ni muhimu siku zimeisha.

Wakili Nashon: Hiyo ndio uliona ya kupanga ugaidi

Shahidi: Kwa sababu walihitajika kwa kazi yao.

Wakili Nashon: Hakuna sehemu mlitumiana kwa ajili ya mishahara.

Shahidi: Ipo

Shahidi: Niwezeshe niweze kumobilaiz nikutane nao Morongo.

Wakili Nashon: Ni watu gani hao?

Shahidi: Sio magaidi

Mahakama. Kicheko…

Wakili Nashon: Ni sahihi ulimwambia Bwire kazi ikibadilika akupigie simu na alikupigia ni sahihi?

Shahidi: Mimi ndio nilimpigia.

Wakili Nashon: Ni lini alikupigia?

Wakili Nashon: Na ni sahihi Bwire kukupiga lilikuwa jambo jema

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Ulirudisha taarifa kwa Kingai kuwa Bwire amekupigia?

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Nashon: Ulishangaa Bwire kukamatwa

Shahidi: Sikushangaa

Wakili Nashon: Kosa la Bwire liko wapi?

Shahidi: Sijui

Wakili wa utetezi John Malya kwa ajili ya mshtakiwa wa pili.

Wakili Mallya: Hizi meseji zinafanana na zile ulizokuwa unasoma?

Shahidi: Ndio

Wakili Mallya: Wapi alipokuita Home boy

Shahidi: Hakuna

Wakili Mallya: Ulimrekodi sauti wakati anakuta home boy

Shahidi: Hakuna

Wakili Mallya: Kwahiyo wewe ndio unajipendekeza kwa Mbowe, ni ushahidi gani ulioleta mahakamani

Shahidi: Ndio anavyoniitaga

Wakili Mallya: Kuna muamala wa tarehe 22/7/2020 una onyesha umetumiwa 199, 000 ulitumiwa kwenye namba 0787555200 ulipokea kutoka kwa nani?

Shahidi: Sikumbuki

Wakili Mallya: Inaonekana ilituma 190, 000 kwa Godson Mmari na baadae ukatuma 7,000 kwenye namba 0787000017 je mmoja ya watuhumiwa?

Shahidi: Hapana

Wakili Mallya: Ni sahihi hii fedha uliyotoa kwa Wakala ni 122,000 na wewe ulisema ulitoa Sh ngapi kwa Wakala?

Shahidi: Nilitoa 300, 000 kutoka mfukoni mwangu nikawapa

Wakili Mallya: Unakumbuka pale kwenye ule mgahawa mlikula

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Mallya: Nani alilipa

Shahidi: Mimi

Wakili Mallya: Ulitoa wapi fedha za kuwalipia

Shahidi: Ni hela za Freeman Mbowe

Wakili Mallya: Uliomba hela za nini

Shahidi: Za kuwasafirisha

Wakili Mallya:  Kuna sehemu ambayo Mbowe alikwambia anakupa pesa ya kuwapa chakula?

Wakili Mallya: Ila wewe ukaona uwalishe magaidi

Wakili Mallya: Kuna neno chakula hapo umelitoa wapi?

Shahidi: Hapana

Shahidi: Nilikuta wanakula na mimi nikajiunga kula, kisha nikalipa

Wakili Mallya:  Twende Kwenye mhamala wa Sh500,000

Wakili Mallya: Nani alikutumia hii pesa

Shahidi: Freeman Mbowe

Wakili Mallya:  Ulitoa Sh300,000

Wakili Mallya:  Ulielezea Mahakama Kwamba Sh200,000 ulimpa nani?

Shahidi: Nilimpa Adamoo na Ling'wenya

Wakili Mallya:  Kuna sehemu umesema kwamba ulitoa Sh ngapi?

Shahidi: Nilikuwa na Cash Mfukoni

Wakili Mallya: Wakati unaaongozwa na wakili ulisema kuna fedha ulizotoa mfukoni ukawapa washtakiwa?

Shahidi: Sikuulizwa

Wakili Mallya: Ulisema baada ya vijana wanne kufika kwa Mbowe alikuwa hakupi tena ushirikiano

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Mallya: Ni sahihi siku unayoenda kumuona alikuwa anatembea na magongo

Shahidi: Sikumuona ilikuwa usiku lakini aliniambia amepigwa na wahuni

Wakili Mallya: Na Unafahamu alikuwa anauguliwa na mtoto

Shahidi: Sifahamu

Wakili Mallya: Unafahamu mwaka jana kulikuwa na uchaguzi mkuu

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Mallya: Kutoka tarehe 20/7,2020 hadi Octoba wakati wa uchaguzi kulikuwa na miezi mitatu ifike uchaguzi

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Mallya: Wakati wa uchaguzi unajua huwa kuna vurugu

Shahidi: Za kawaida

Wakili Mallya: Mtu kuwa na walinzi ni kosa?

Shahidi:Kuwa na mlinzi sijui kama ni kosa au kosa

Wakili Mallya: Umempa mtu hela umemwambia nenda kwa Mbowe ukawe mlinzi ni kosa?

Shahidi: Kwa wakati huo sio kosa

Wakili Mallya: Hao mtu tatu au nne uliwaambia wakafanye nini

Shahidi: Shahidi Kuambatana kazi ya Ulinzi

Wakili Mallya: Nionyeshe kwenye meseji mahali Mbowe anasema anaenda kuvunja Sheria

Shahidi: Hakuna

Wakili Mallya: Ilikuwa una wajibu wa kuwasaidia polisi kukusanya ushahidi ili uhalifu wa Mbowe ufahamike

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Mallya: Nisomee meseji hii

Shahidi: Usiwe unatumia namba yako kutuma pesa tumia wasaidizi wako au Wakala

Wakili Mallya:  Umemuelekeza Mbowe cha Kufanya, ni sahihi akitekeleza unachosema haitoonekana namba yake

Shahidi: Ni sahihi

Wakili Mallya: Ni swali langu la mwisho kwa jioni hii

Mheshimiwa Jaji muda umetutupa mkono naomba ahirisho hadi kesho nitakapoendelea na maswali kwa shahidi kwa niaba ya mshtakiwa wa pili.

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Hatuna pingamizi Mheshimiwa Jaji.

Jaji: Kutokana na muda na kufuatia maombi ya Wakili wa utetezi John Mallya naahirisha kesi hii hadi kesho Januari 28, 2022 saa tatu asubuhi kwa ajili ya shahidi wa 12 kuendelea kuhojiwa na upande wa utetezi.