Mahakama yachambua mfumo wa maisha ya Mengi ikiamua mirathi (4)

Muktasari:
- Katika kesi ya mirathi ya mfanyabiashara maarufu na mmiliki wa kampuni za IPP, Reginald Mengi, jana tuliona jinsi kikao cha ukoo kilivyokataa kutambua wosia wa mwisho wa tajiri huyo kwa madai kwamba hakuna mwanafamilia aliyeushuhudia.
Katika kesi ya mirathi ya mfanyabiashara maarufu na mmiliki wa kampuni za IPP, Reginald Mengi, jana tuliona jinsi kikao cha ukoo kilivyokataa kutambua wosia wa mwisho wa tajiri huyo kwa madai kwamba hakuna mwanafamilia aliyeushuhudia.
Katika kesi hiyo watu wanne walifungua maombi ya kutaka Mahakama iwathibitisha kuwa wasimamizi wa mirathi kupitia wosia ambao Mengi alimrithisha mali zake zote mke wake wa pili, Jacqueline Ntuyabaliwe na watoto wake pacha.
Kufuatia maombi hayo, watoto wa marehemu waliweka zuio la mchakato huo hadi mahakama itakapowasikiliza na kuamua mapingamizi yao. Endelea…
Baada ya kupitia ushahidi na majumuisho ya mawakili wa pande zote, mahakama ilifanya uchambuzi wa ushahidi na kutoa msimamo wake katika kila hoja iliyoletwa mbele yake.
Katika utaratibu wa sheria, kabla ya kuamua shauri la wosia unaogombaniwa, mahakama huanza kwa kuchagua sheria itakayoitumia kuamua kesi ya mirathi husika kabla ya kuamua kuhusu uhalali wa wosia na mambo mengine yanayohusu usimamizi wa mirathi ya marehemu.
Nchini Tanzania kuna sheria tatu zinazoongoza masuala ya mirathi na usimamizi wa mirathi – Sheria Bunge (Statutory Law), Sheria za Kimila (Customary Law) na Sheria za Kiislamu (Islamic Law).
Uchaguzi wa sheria itakayotumika kuamua shauri la wosia unaobishaniwa, huja baada ya Mahakama kuchambua mfumo wa maisha ya mwenye wosia na kujiridhisha aina ya mfumo uliotawala zaidi maisha yake.
Kama aliishi kwa kufuata mwongozo wa dini ya Kiislamu, basi Mahakama hutumia Sheria ya Kiislamu kuamua shauri lake la mirathi pindi anakapofariki na ukatokea mvutano katika mirathi yake.
Sheria Bunge (Statutory Law) ambayo kwa Tanzania hutumiwa Indian Succession Act au Sheria ya Mirathi ya Serikali, hutumika kwa Wakristu na watu wengine wote ambao hawaongozwi na Sheria ya Kiislamu au ya Kimila, ambayo hutumika kwa watu walioishi zaidi kwa kufuata mila, desturi na tamaduni za kabila au jamii yao.
Mahakama zimeandaa vigezo vya kuamua chaguo sahihi la sheria itakayotumika kuamua kuhusu wosia au usimamizi wa mirathi wenye mgogoro.
Kigezo cha kwanza ni kuchambua mfumo wa maisha (Mode of Life) ya marehemu na cha pili ni kujua nia ya kuandika wosia (Intention of Test—pale mtu anapoacha wosia, anapofanya matamko ya maandishi au ya mdomo kuhusu usimamizi wa mali zake wakati akiwa hai).
Mahakama huzingatia ushahidi ulioletwa mahakamani na pande zote mbili kupata majibu ya vigezovyote viwili na hatimaye huamua ni sheria ipi itumike katika usimamizi wa mirathi ya marehemu.
Maisha ya sura mbili Katika kesi ya mirathi ya Mengi, Mahakama ilichagua kuongozwa na kipimo cha mfumo wa maisha aliyoishi marehemu ili kujua sheria ipi ingefaa kuamua suala la usimamizi wa mirathi yake.
Jaji Yose Mlyambina aliyesikiliza kesi hiyo alisema uamuzi wa sheria ipi iongoze suala hilo unaweza kujulikana kutoka kwenye aina au mfumo wa maisha ya marehemu.
Alisema ushahidi uliotolewamahakamani ulionyesha wazi kwamba maisha ya marehemu Mengi yalikuwa na sura mbili.
“Kwa kiasi fulani yalikuwa katika mfumo wa kimila na kiasi fulani katika mfumo wa maisha ya kisasa, vyote katika kiwango kinacholingana. “Hii inamaanisha kuwa Sheria ya Kimila au Sheria Bunge inaweza kutumika katika mirathi ya marehemu Mengi,” alisema Jaji Mlyambina.
Hata hivyo, sheria zote mbili haziwezi kutumika kwa kuwa sheria zilizopo na maamuzi ya Mahakama yaliyowahi kutolewa siku za nyuma vinataka sheria moja tu itumike katika kuamua mgogoro waJaji Mlyambina anakiri kuwa Mahakama ilikabiliwa na ugumu wa kipekee pale ilipothibitika kuwa Mengi aliishi, aliheshimu na kutekeleza kwa vitendo mila na desturi za Kichaga kwa kiwango karibu sawa na jinsi alivyoishi, kuheshimu na kutekeleza kwa vitendo maisha ya kisasa kama Mkristo.
Katika hatua hiyo jaji anasema Mahakama hupima ni mfumo upi kati ya ule wa maisha ya kimila na wa maisha ya kisasa ulitawala zaidi maisha ya marehemu. Mahakama inaporidhika kuwa mfumo wa maisha ya kimila ulitawala zaidi mfumo wa maisha ya marehemu, hutamka kuwa sheria ya kimila ndiyo itakayotumika katika mirathi ya marehemu.
Pale inaporidhika kuwa mfumo wa maisha ya kisasa ulitawala sehemu kubwa ya maisha wa marehemu, mahakama itatamka kuwa Sheria Bunge itumike. Mahakama ilisema kwa mujibu wa shahidi wa kwanza, Sylvia Mushi (katibu wa kampuni ya IPP) pamo[1]ja na mtoto wa Mengi, Abdiel na kaka yake, Benjamin, marehemu aliheshimu na kutekeleza mila, des[1]turi na utamaduni wa Kichaga kama sehemu muhimu ya maisha yake sambamba na mfumo wa maisha ya kisasa wakati wa uhai wake.
Kwa mujibu wa ushahidi wao, marehemu Mengi alikuwa mwe[1]nyekiti wa ukoo wa Mengi; aliwapa watoto wake wote majina ya Kichaga; kama walivyo Wachaga wengine, pia alitembelea sehemu za wazee huko Machame, Kilimanjaro kila Desemba.
Pia eneo la makaburi ya ukoo wake yalikuwa Machame na alizikwa kati[1]ka makaburi hayo na kwamba tarati[1]bu za Kikristu na za kimila zilifuatwa katika mazishi yake.
Ingawa pia alifunga ndoa ya Kikris[1]tu na mke wake wa kwanza, tamadu[1]ni na mila za Kichaga zilifuatwa na kuheshimiwa.
Ushahidi ulionyesha pia kuwa Mengi alitembelea mara kwa mara maeneo ya mababu zake Machame na alijenga nyumba yake huko. Ushahidi unaeleza kuwa Men[1]gi alizaliwa na kukulia Machame na alishiriki katika kanuni zote za Kichaga, zikiwemo kuchinja ndafu na kusimika mkuu wa familia, maarufu kama ‘kuvisha koti.’
Kutokana na ushahidi huo, Jaji Mlyambina akahitimisha kuwa kuto[1]kana ushahidi ulioletwa mbele yake, hakukuwa na shaka kuwa Mengi ali[1]tekeleza mila, desturi na utamaduni wa Kichaga kama sehemu muhimu ya maisha yake.
Akaongeza kwamba mfumo wa maisha ya kisasa uliendelea kuwa sehemu muhimu ya mfumo wa mai[1]sha ya marehemu Mengi. “Mengi alikuwa mtu aliyependa mfumo wa maisha ya kisasa (mor[1]denist),” alisema.
Mahakama ilisema hilo liliungwa mkono na ushahidi kuwa alifunga ndoa ya Kikristu na mke wake wa kwanza na pia alifunga ndoa ya Kiserikali na mke wake wa pili mwa[1]ka 2015 katika Wilaya ya Kinondoni na baadaye alikwenda Mauritius kufanya sherehe ya harusi.
Pia aliwabatiza watoto wake kwa kuwapa majina ya Kikristo na alitu[1]mia sehemu kubwa ya maisha yake ya utu uzima jijini Dar es Salaam ambalo ndilo kitovu cha maisha ya kisasa kuliko nyumbani kwa mababu zake Machame.
Hoja nyingine ni kuwa taratibu za Kikristu zilifuatwa wakati wa mazishi yake na alikuwa akifanya uchunguzi wa afya yake Uingereza, Afrika Kusini na Umoja wa Falme za Kiarabu.
Pia kwa asili ya shughuli zake kama mmoja wa wafanyabiashara tajiri Tanzania na mwenyekiti wa kam[1]puni za IPP, haikuwa rahisi kwake kukwepa kabisa maisha ya kisasa. Uamuzi wa Mahakama Jaji Mlyambina alisema japokuwa, kwa ukadiriaji wa Mahakama, Mengi aliishi mfumo wa maisha mchang[1]anyiko (hybrid mode of life), ilion[1]ekana kuwa mfumo wa maisha ya kisasa ulitawala zaidi mfumo wake wa maisha, hivyo Mahakama iliamua kutumia sheria inayofaa kulingana na mfumo wa maisha wa marehemu.
“Kwa kuwa ni hitimisho la mahaka[1]ma hii kuwa mfumo wa maisha ya kisasa ulitawala mfumo wa maisha ya Dk Reginald Abraham Mengi kuliko mfumo wa maisha ya kimila, mahakama hii inatamka kuwa She[1]ria ya Bunge ndiyo itakayotumika katika kuamua shauri la usimamizi wa mirathi ya marehemu Reginald Mengi, ikiwemo kuamua uhalali wa wasia wake wa mwisho,” alisema Jaji Mlyambina.
Baada ya hapo Mahakama ilijikita katika kuamua kama wosia wa mare[1]hemu Mengi aliouandika Agosti 17, 2017 Dar es Salaam uliandikwa kiha[1]lali na kama wosia huo uliodaiwa kuandikwa Agosti 17, 2017 na Mengi ulikuwa kwa usahihi. Itaendelea kesho