Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Rais Samia afanya uteuzi

Rais Samia afanya uteuzi

Muktasari:

  • Rais Samia Suluhu Hassan, leo Septemba 10, 2021 amemteua Dk Stergomena Tax kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan, leo Septemba 10, 2021 amemteua Dk Stergomena Tax kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Taarifa iliyotolewa leo Ijumaa Septemba 10, 2021 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu imesema Tax ameteuliwa kutoka kwenye nafasi kumi za wabunge wa kuteuliwa na Rais.

Kabla ya uteuzi huo alikuwa Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) ambaye amemaliza muda wake mwezi Agosti 2021.

Mbunge huyo ataapishwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.