Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Sheikh Mjaila: Kukosa imani chanzo cha kuongezeka matukio ya mauaji

Wanafunzi wa shule ya sekondari Handeni wakiwa wamebeba sadaka ya nyama waliopewa kutoka msikiti mkuu wa Ijumaa wilayani humo jana katika kuadhimisha sikukuu ya Eid Al Adha.Picha na Rajabu Athumani

Muktasari:

Hivi karibuni kumeibuka matukio ya watu kuuana katika maeneo mbalimbali kwa kupigana risasi, kuchomwa moto na kunyongwa hali inayotishia amani.

Handeni. Imeelezwa kuwa kitendo cha wananchi kuacha kufanya ibada na kufuata miongozo ya dini, ndio chanzo cha kutokea matukio mbalimbali ya mauaji, kwani waumini wamekosa hofu kwenye mioyo yao na wala hawamuogopi Mungu.

Hayo yamesemwa na imamu wa msikiti mkuu wa Ijumaa wilayani Handeni mkoani Tanga, Alhaj Sheikh Ali Mjaila, kwenye ibada ya swala ya Eid Al Adha mjini hapa leo Julai 21 na kusema kuwa, kila mmoja amrudie Mungu na kufahamu kuwa kufanya hayo ni makosa kutokana ma maandiko ya dini zote.

Amesema licha ya matukio ya watu kuuawa maeneo mbalimbali nchini kwa kupigana risasi, kunyongana na hata mapigano ya wakulima na wafugaji ni ukosefu wa imani kwenye mioyo yao na kutokuwa na hofu ya kumuogopa Mungu, hivyo watu wajitahidi kumrudia Mungu ili kurejesha amani za familia zao.

"Tunasikia kwenye vyombo vya habari kila kukicha mara huko wameuana, amepigwa risasi, amechomwa moto, amenyongwa, haya matukio zamani ni nadra kuyasikia, hii inasababishwa hatuna hofu ya Mungu kwenye mioyo yetu na tumekosa imani, tumrudie Mungu, tupendane na tujenge hofu hili litarejesha  amani kwenye nyumba zenu," amesema Alhaj Mjaila.

Kuhusu kuwepo ugonjwa wa corona Sheikh Mjaila amesema watu wanakumbushwa kuhusu usafi wa mazingira na miili yao, kila mmoja ajiulize ni kwa nini anasisitizwa anawe mikono na sabuni, kwa sababu wananchi wanajisahau kuhusu usafi wao.

"Ina maana kama utaepuka mikusanyiko isiyo ya lazima, utanawa mikono yako kwa maji safi na sabuni tayari umefuata kanuni za afya za usafi wako binafsi pamoja na mazingira hivyo kuepuka huu ugonjwa, haya ni makumbusho kwamba tunatakiwa kuwa wasafi muda wote.

Muumini Halfa Kaduka amesema Serikali na viongozi wa dini waongeze msisitizo wa kihakikisha sheria za usafi zinafuatwa ili kuweza kuepukana na ugonjwa wa corona.